HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » WAZIRI AGGREY MWANRI AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI KATAVI

DSC00508
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akimkabidhi Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Aggrey Mwanri Vitabu vya Mafanikio ya Miaka 50 ya Uhuru Mkoa wa Rukwa mara baada ya kuvizindua katika moja ya matukio ya shughuli zake za kikazi mkoani Rukwa. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Dkt. Rajab Rutegwe.
………………………………………………………….
NA KIBADA KIBADA WA FULLSHANGWE-KATAVI
Watumishi  wote wa umma wametakiwa kuwajibika vyema katika maeneo yao ya kazi  na kila mmoja kwa nafasi yake katika utoaji wa huduma pale alipo ili kuleta maendeleo yanayokusudiwa  kwa ujenzi wa Taifa.
Akizungumza katika kikao cha majumuisho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano idara ya  Maji Wilayani mpanda Mkoani Katavi mara baada ya kumaliza ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda na Wilaya ya Mlele Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa Aggrey Mwanri alihimiza uwajibikaji na utendaji kazi  mzuri kwa kila mtumishi wa umma na kila mtu kwa nafasi yake katika jamii iwapo atatimiza wajibu ataweza kufanikisha suala la kuleta maendeleo kwa Taifa na yeye Mwenyewe.
Amesema uzalendo ni muhimu sana katika utendaji wa Kazi bila uzalendo katika kazi hakuna mafanikio, mataifa yote yaliyofanikiwa kiuchumi ni kutokana na uzalendo wa watu wake kuipenda nchi na kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu mkubwa ili kufikia mafanikio waliyojiwekea.
Alisema watumishi wanatakiwa wachape kazi kwelikweli ili iwe mfano kwa wananchi wengine katika maeneo wanaokofanyia huduma ya utumishi wao,wajitume kwa nguvu zote.
Amesema serikali ina miundo mbinu mizuri sana  iwapo wananchi wote wangekuwa na uzalendo wa kuisimamia  kwa pamoja na kufanya kazi kwa nguvu kwa kujituma bila kusukumwa  Taifa lingepiga hatua kubwa ya maendeleo.
Katika ziara yake wilayani mpanda na Mlele  ametembelea na kukagua miradi ya maendeleo kwa lengo la kuona fedha zinazoletwa kwenye Halmashauri kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama zinasimamiwa vizuri,na miradi iliyotekelezwa inalingana na thamani ya fedha yenyewe iliyotolewa na serikali kuu.


CHANZO: FULL SHANGWE

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: