Amini na Linah wakiwa kazini katika pozi tofauti
Wakati wakiwa katika fununu za kuwepo kwa harakati za kufunga ndoa baina ya wasanii wa kizazi kipya Bongo, Amini na Esterinah Sanga muite Linah, Mume huyo ameibuka na kupasua jipu kuwa hana mpango wowote wa kumvisha pete ya uchumba mwanadada huyo.
Amini
Amini alisema kuwa kipindi cha nyuma aliwahi kuwazia suala hilo lakini hivi sasa hana ndoto kabisa.
”Ukweli ni kwamba sifikirii lolote kuhusu kumvisha pete Linah watu wengi walidhani labda ningemvisha pete ya uchumba jumapili iliyopita pale maisha club kwenye ‘Birthday Party’
yake lakini haikuwa hivyo,” Alisema Amin na kuongeza kuwa pamoja na
kutokuwa na mawazo hayo lakini anachofanya ni kumuweka karibu Linah hasa
kikazi wakati mikakati mingine ya msingi wakiendelea kupanga. (Picha na Harakati za Bongo)




No comments:
Post a Comment