Hii ndio hali halisi ya ombaomba huyu tulimfuma mida ya saa saba mchana huu akiwa anaanika juani pesa ili zikauke. Na pia kulikuwa na pesa nyingine alizokuwa nazo yasemekana pesa za noti tu zilikuwa ni zaidi ya elfu sabini. Kiukweli hali hii inasikitisha sana kuona ombaomba anakuwa na shilingi zipatazo kama elfu tisini kwa nusu siku.
Swali langu je, ikifika jioni hatakuwa na shilingi ngapi? maana kipato cha huyu ombaomba kinamzidi hata mfanyakazi wa serikali mara tano yake kwa siku kulinganisha na kiwango cha mshahara wa kati wa mfanyakazi wa serikali.




No comments:
Post a Comment