HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Kishindo Kenya: Matokea vituo 50 yainga dosari

Afisa wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya akifanya kazi ya kuhesabu kura zilizowasilishwa katika kituo cha kuhesabu kura mjini Nairobi. Picha na AFP  

Wakati leo ikiwa ni siku ya tano tangu kufanyika Uchaguzi Mkuu  nchini Kenya, Muungano wa CORD, umeitaka Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini humo (IEBC), kusitisha shughuli ya kuhesabu kura kwa madai kuwa umefanyika udanganyifu.
Jana mashirika ya kijamii yalikwenda mahakamani kufungua kesi ili kuitaka Mahakama Kuu kusitisha shughuli inayoendelea ya kuhesabu kura.
Mahakama Kuu ilitakiwa kutoa uamuzi wa kesi hiyo na mashirika hayo ya kijamii, ambayo pia yanashinikiza zoezi linaloendelea la kuhesabu kura za urais katika Ukumbi wa Bomas kusitishwa.
Makundi hayo yalidai kuwa IECB  inakwenda kinyume na Katiba  ya Kenya inayoelekeza kwamba kura kuhesabiwa kwa njia ya elektroniki.
Kufuatia kesi hiyo, majaji  watatu waliteuliwa kuisikiliza ambao ni Jaji Isaac Lenaola, Jaji David Majanja na Jaji Weldon Korir.
Hata hivyo, majaji hao walisema kwamba mahakama hiyo  haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.
Wakati makundi hayo yakichukua hatua hiyo, tume hiyo ya uchaguzi nayo ilisema  kuwa idadi kubwa ya kura zilizoharibika zilitokana na hitilafu katika mtambo wake, ambao ulikuwa ukiongeza idadi ya kura hizo mara nane.
Wakati hayo yakiendelea, hadi sasa matokeo ya kura za urais Uhuru Kenyatta ana kura 5,219,456, huku mpinzani wake wa karibu,  Raila Odinga akiwa na 4,630,161 ya kura zilizohesabiwa.
Taarifa nyingine kutoka nchini humo zilisema kuwa watu wameanza kurejea kazini licha ya bei za bidhaa kuanza kuwa ghali kutokana na wafanyabiashara kupata hofu kwenda maeneo jirani kununua vyakula hadi matokeo yatakapotangazwa.
Akizungumza katika Ukumbi wa Bomas jana, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IECB), Ahmad Isaack Hassan aliwataka wananchi kutokuwa na wasiwasi kwa kuwa kura zinahesabiwa vizuri na matokeo yatatolewa  baada ya kumalizika kuhesabiwa.
‘’Najua mnachoka kusubiri, lakini zoezi linaendelea vizuri na hakuna suala la wizi lililotokea mpaka sasa, wananchi wa Kenya tuaminiane kwa hili,” alisema.
Aliongeza kuwa kura zanahesabiwa moja baada ya nyingine chini ya ulinzi mkali, hivyo hakuna anayependelewa, wala anayeonewa na haki inatendeka.
Aliwataka wananchi waendelee na shughuli zao za kila siku kwa sababu zoezi karibia litakamilika muda siyo mrefu na pindi tu wakimaliza kuhesabu wanatangaza matokeo hayo.
Katika hatua nyingine habari kutoka katika kituo cha kuhesabia kura zinaeleza kuwa matokeo yatachelewa kutangazwa kutokana na matatizo yaliyojitokeza katika vituo vya kupigia kura 50.


MWANANCHI

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: