Eneo
la tukio ambapo jengo la ghorofa zaidi ya 10 liliporomoka jana asubuhi
na hadi kufikia saa sita mchana leo maiti 18 zilikuwa zimeopolewa na
watu wanne wakiwemo wakandarasi waliokuwa wanajenga pamoja na wahandisi
wa halmashauri ya wilaya ya Ilala wanashikiliwa na polisi, wakati wawili
wanaendelea kusakwa ikiwa ni pamoja na mjenzi ambaye kapewa masaa 12
kujisalimisha. Kuna habari kwamba jengo hilo refu kulia pia linajengwa
na mkararasi aliyejenga hili lililoporomoka na kila aliye sehemu hii
analiangalia kwa jicho la wasiwasi.(Picha na Full Shangwe)
Rais
Kikwete akiwa eneo la tukio tena leo, baada ya kutembelea jana, akitoa
maagizo kwa Kamanda wa Kanda maalumu ya Dar es salaam Suleiman Kova
kwamba kila aliyehusika na ujenzi wa jengo hilo kuanzia mchoraji,
msimamizi na mjenzi wahojiwe na wawajibishwe wakipatikana na kosa
Rais Kikwete akiongea na viongozi wa msikiti wa Shia ithnaasheri wakati anaondoka eneo la tukio
Mkuu
wa Polisi Kanda Maalum Mkoa wa Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova
akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika eneo la Tukio kwenye
jengo lililoanguka jana maeneo ya Posta jijini Dar es salaam na
kusababisha vifo vya watu, Majeruhi na Uharibifu wa mali, Mpaka mchana
huu imethibitika ni watu 20 wamenasuliwa kutoka katika kifusi cha jengo hilo
na majeruhi kadhaa, kazi ya uutafuta miili ya watu waliopoteza maisha
inaendelea mpaka sasa katika eneo hilo huku vikosi vya ulinzi na usalama
pamoja na taasisi mbalimbali vinashirikiana kwa pamoja kuhakikisha
vinakamilisha kazi ya kutafuta miili ya watu waliopoteza maisha katika
trukio hilo. 
Mwenyekiti
wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba akihojiwa na
mwandishi wa habari wa TBC Grace Kingalame wakati alipotembelea eneo la
tukio na kujionea hali halisi ya uokoaji.








No comments:
Post a Comment