HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Yaliyojiri kwenye Ziara ya Rais Xi Jinping wa China


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais wa China Xi Jinping wakiweka mashada ya maua katika makaburi ya wataalamu wa China waliofariki wakati wa ujenzi wa Reli ya TAZARA.Viongozi hao waliweka mashada hayo ya maua katika makaburi hayo yaliyopo katika kijiji cha Majohe,Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mke wa Rais wa China Mama Peng Liyuan wakiweka maua katika makaburi ya wataalamu wa China waliofariki wakati wa ujenzi wa Reli ya TAZARA huko katika kijiji cha Majohe,Ukonga nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wa Rais Xi Jinping wakishuhudia(picha na Freddy Maro). 
IMG_8560
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar alipowasili katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, alipokuwa na Mkutano na Rais wa China Xi Jinping,leo asubuhi.
[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_8577 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping,katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam,walipokutana kwa mazungumzo ya Kiutendaji. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akimtambulisha Waziri wa Fedha,Uchumi na Mipango ya Maendeleo Omar Yussuf Mzee,kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping,katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam,walipokutana kwa mazungumzo ya Kiutendaji.
 IMG_8613  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping,katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam,walipokutana leo asubuhi ikiwa ni hatua ua ushirikiano katika nchi mbili hizi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_8622
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiagana na Balozi Mdogo wa China anyeishi Zanzibar Bibi Chen Yiman,baada ya mazungumzo na Rais wa China Xi Jinping, katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
 
 Rais wa Tanzania akitoa Speech kwa Xi Jinping Rais wa China
 
Rais wa ChinaXi Jinping akitoa speech ambayo Rais Kikwete alikuwa anaisikiliza kiumakini
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ufunguo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping wakati wa makabidhiano ya ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Ukumbi huo umejengwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya China na Tanzania.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa China Mhe.Xi Jinping wakiangalia picha za matukio mbalimbali yanayohusu historia ya ushirikiano kati ya China na Tanzania katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere wakati wa sherehe za makabidhiano ya ukumbi huo jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa China, Mhe. Xi Jinping pamoja na mkewe katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere muda mfupi baada ya sherehe za ufunguzi wa ukumbi.

8E9U1655 
 Rais Dkt Jakaya Mrisho kikwete wakigonganisha Glasi na Rais Xi Jinping wa China wkati wa dhifa ya kitaifa iliyofanyika ikulu jijini Dar Es Salaam jana jioni.Rais Xi Jinping wa China yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.Ni ziara yake ya kwanza barani Afrika tangu achaguliwe kuliongoza taifa la China hivi karibuni na Tanzania inakuwa nchi ya kwanza kuitembelea barani Afrika(picha na Freddy Maro)


 Picha na Ramadhan Othman Freddy Maro

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: