Rais
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais wa China Xi Jinping
wakiweka mashada ya maua katika makaburi ya wataalamu wa China
waliofariki wakati wa ujenzi wa Reli ya TAZARA.Viongozi hao waliweka
mashada hayo ya maua katika makaburi hayo yaliyopo katika kijiji cha
Majohe,Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete na mke wa Rais wa China Mama Peng Liyuan
wakiweka maua katika makaburi ya wataalamu wa China waliofariki wakati
wa ujenzi wa Reli ya TAZARA huko katika kijiji cha Majohe,Ukonga nje
kidogo ya jiji la Dar es Salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni
wa Rais Xi Jinping wakishuhudia(picha na Freddy Maro).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar alipowasili katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, alipokuwa na Mkutano na Rais wa China Xi Jinping,leo asubuhi.
[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping,katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam,walipokutana kwa mazungumzo ya Kiutendaji. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein,(katikati) akimtambulisha Waziri wa Fedha,Uchumi na Mipango ya
Maendeleo Omar Yussuf Mzee,kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi
Jinping,katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es
Salaam,walipokutana kwa mazungumzo ya Kiutendaji.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping,katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam,walipokutana leo asubuhi ikiwa ni hatua ua ushirikiano katika nchi mbili hizi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiagana na Balozi Mdogo wa China anyeishi Zanzibar Bibi Chen Yiman,baada ya mazungumzo na Rais wa China Xi Jinping, katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Rais wa Tanzania akitoa Speech kwa Xi Jinping Rais wa China

Rais wa ChinaXi Jinping akitoa speech ambayo Rais Kikwete alikuwa anaisikiliza kiumakini
Rais
Dkt Jakaya Mrisho kikwete wakigonganisha Glasi na Rais Xi Jinping wa
China wkati wa dhifa ya kitaifa iliyofanyika ikulu jijini Dar Es Salaam
jana jioni.Rais Xi Jinping wa China yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya
siku mbili.Ni ziara yake ya kwanza barani Afrika tangu achaguliwe
kuliongoza taifa la China hivi karibuni na Tanzania inakuwa nchi ya
kwanza kuitembelea barani Afrika(picha na Freddy Maro)
Picha na Ramadhan Othman Freddy Maro



No comments:
Post a Comment