Baada ya Bunge kuahirishwa jana, nje ya ukumbi hali haikuwa nzuri
baina ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Same
Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela.
Mtafaruku huo uliibuka baada ya Kilango kusikika akimtuhumu Lissu
kwa uchochezi, akisema kwamba amekuwa mbunge pekee anayeongoza kwa
vurugu. Maneno hayo hayakumfurahisha Lissu ambaye alishindwa kuvumilia na
kumgeukia Kilango kwa nguvu huku baadhi ya wabunge wakishuhudia na
wengine wakimzuia Lissu.
No comments:
Post a Comment