Picha ya Rais wa Marekani, Barrack Obama ikiwa imepambwa sambamba na
bendera ya taifa hilo na ya Tanzania kwenye Mtaa wa Ohio katikati ya
Jiji la Dar es Salaam leo. Obama anawasili nchini kesho kwa ziara ya
siku mbili.
Mtaa wa Ohio ukipendeza kwa usafi. Ohio ni moja ya majimbo ya Martekani.
Endelea kutizama maeneo mengine kwa kubofya hapa chini
Hali ilivyo kwa sasa eneo la Posta mpya jijini Dar es Salaam baada
ya wafanyabiashara ndogo ndogo machinga na wauza magazeti na vocha
eneo hilo kuondolewa na mgambo wa jiji katika zoezi la kusafisha
jiji kwa ajili ya ugeni huo mkubwa nchini
Wafanyakazi wa Manispaa ya Kinondoni, wakiwa katika pilikapilika za
kufanya usafi jana katika taa za kuongozea magari Ubungo, ikiwa ni
maandalizi ya ujio wa Rais wa Marekani, Barrack Obama anayetarajia
kuwasili leo nchini kwa ziara ya siku mbili, ambapo pia atatembelea
mitambo ya umeme ya Symbion iliyopo Ubungo, Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Manispaa ya Kinondoni, wakifanya usafi leo katika taa za
kuongozea magari Ubungo, ikiwa ni maandalizi ya ujio wa Rais wa
Marekani, Barrack Obama anayetarajia kuwasili leo nchini kwa ziara ya
siku mbili, ambapo pia atatembelea mitambo ya umeme ya Symbion iliyopo
Ubungo, Dar es Salaam.
PICHA NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA



No comments:
Post a Comment