Baada ya tangazo la jeshi sherehe zililipuka kote nchini humo huku
wapinzani wengi wa Morsi wakiona hatua ya jeshi kama ushindi wao
Watoto, akina mama , wazee , wote wajitoa katika barabara za nchi kusherehekea
Wanajeshi nao walikuwa kote kushika doria mjini Cairo, angani na ardhini
licha ya taarifa kusema kuwa baadhi ya watu walijeruhiwa
Endelea kutizama tukio hapa kwa kubofya hapa chini
Kabla ya taarifa ya jeshi ya kumwondoa mamlakani Morsi, pande pinzani
zilikuwa zimefanya maandamano kumuunga na kumpinga mkono Morsi
Fataki ishara ya sherehe zilizofanyika usiku kucha mjini Cairo
Vijana ambao ndio wengi waliokuwa wanalalamika kuwa Morsi alikuwa anakumbatia sheria kali za kiisilamu
Wengi pia walimtuhumu kwa kuhujumu faida za mapinduzi ya kiraia yaliyofanyika kumwondoa mamlakani rais Hosni Mubarak
BBC SWAHILI



No comments:
Post a Comment