HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » BUNGE LA KENYA LAPITISHA MUSWADA WA UGAVI WA MALI KATI YA WANANDOA BAADA YA KUTALIKIANA


BUNGE  la nchini Kenya leo Novemba 13 limepitisha muswada wa ugavi wa mali kati ya wanandoa baada ya kutalikiana.
Muswada huo unaeleza kwamba mwanamume au mwanamke atapata sehemu ya mali aliyochuma wakati wa ndoa iwapo wataamua wanandoa watamua  kuachana.
Katiba ya sasa inaeleza wazi kuhusu haki sawa kati ya wanandoa kabla,wakati na hata baada ya kuvunjika ndoa. inaeleza kwamba mali inayomilikiwa wakati wa ndoa itagawanywa nusu kwa nusu baina ya mume na mke iwapo wataachana.

 ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI


Wabunge wanawake nchini  humo  wanataka muongozo usalie kama ulivyo,Idadi kubwa ya wabunge wanaume walipiga kura kwa uwingi wa kura 87 dhidi ya wabunge wanawake 28 kuibadili sheria hiyo.
Sehemu kubwa ya wabunge wanawake waliwashutumu wenzao wanaume kwa kupitisha mswada huo ambao wameutaja kwenda kinyume na katiba.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: