HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » KIJANA APATA KICHAPO CHA MBWA MWIZI BAADA YA KUIBA KWENYE GARI

  Link Mbaga baada ya kula kichapo cha nguvu kutoka kwa wananchi wenye hasira kali.
 Mbaga akisulubiwa na wananchi.

 ENDELEA KUTIZA MATUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI


 Gari aina ya Toyota Harrier walilotaka kuiba power window Mbaga na wenzake.
 Mbaga akiwa hoi baada ya kichapo.
 Polisi wakijaribu kuchukua maelezo ya mtuhumiwa baada ya kuwasili eneo la tukio.
 Polisi wakimbeba Mbaga kumpeleka kwenye gari la polisi.
Safari ya kuelekea Mwananyamala ikaanza.


MKAZI mmoja wa Sinza Lion jijini Dar, Link Mbaga (25) Jumanne iliyopita alinaswa maeneo ya Sinza Afrikasana na kuchezea kichapo kutoka kwa watu wenye hasira akidaiwa kutaka kuiba vifaa vya kwenye gari aina ya Toyota Harrier, Ijumaa limeinyaka.

Shuhuda wa tukio hilo ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini, alisema Mbaga na wenzake wanne wanaodaiwa kuwa ni vinara wanaounda mtandao wa kuiba power window kwenye magari walifika eneo la tukio wakiwa ndani ya gari aina ya Toyota Noah
 “Lengo lao lilikuwa ni kuiba kwenye gari la mteja wa Hospitali ya Marie Stop lililokuwa limeegeshwa nje ya hospitali hiyo,” alisema shuhuda huyo.
 Shuhuda huyo alisema Mbaga na wenzake walifanikiwa kulitoboa gari hilo na kuchukua simu mbili pamoja na kompyuta mpakato ‘laptop’.
“Kabla ya kumalizia zoezi lao mlinzi wa hospitali hiyo aitwaye Jonas Mwakajinga aliwasikia ndipo alipofika na kuwakurupusha,” kimesema chanzo hicho.
 Mbali na kusema hivyo, Mbaga alidai kwamba ameoa na mkewe anaitwa Fausani na kabla ya kufika hapo alikuwa na rafiki yake wakinywa pombe Mlimani City.
 Mbaga aliokolewa na askari waliotokea na kumbeba msobemsobe hadi katika Kituo cha Polisi cha Mwananyamala.
Kutokana na hali mbaya ya mtuhumiwa huyo, askari hao walilazimika kumpeleka Hospitali ya Mwananyamala ili aweze kupata matibabu.

HABARI NA GPL

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: