
Bendera ya Ufilipino ikiwa chini jengo lililoporomoka
Idadi ya watu waliofariki kufuatia kimbunga cha Haiyan kilichopiga nchini Ufilipino na Vietnam inaweza kufikia 10,000.
Mpaka
sasa kimbunga hicho kimeshaua watu 1,200 nchini Ufilipino na kuwaacha
wengine wakiwa wamejeruhiwa. Wengine wamekufa kwa kuzama ama kuangakiwa
na majengo. Takriban watu milioni 4 wanaaminika kuathiriwa na kimbunga
hicho kinachoaminika kuwa kibaya zaidi kupiga eneo hilo. Tazama baadhi
ya picha za jinsi kimbunga hicho kilivyosababisha maafa makubwa.

Mama akilia pembeni ya mwili wa mwanae aliyefariki baada ya kutafuta hifadhi kanisani

Wanakijiji wakitupa gunia la mchanga kwenye paa la nyumba katika jimbo la Quang Nam, Vietnam


Kimbunga cha Haiyan kinavyoonekana kwenye picha

Miili ikiwa imelazwa kwenye kanisa

Msichana akisimama kutathimini hasara iliyotokana na kimbunga hicho

Mwanajeshi wa Vietnan akiwa amembeba mtoto wa kike kutoka kwenye roli baada ya kuokolewa na kupelekwa sehemu salama

Picha hii inaonesha jinsi mji wa Tacloban ulivyoharibika vibaya kutokana na kimbunga hicho

Picha inayoenesha eneo hili lilivyofurika maji

Takriban watu milioni 4 wanadaiwa kuathiriwa na kimbunga hicho nchini Ufilipino

Wakazi wa Phu Yen, Vietnam wakitengeneza magunia ya mchanga kujiandaa na kimbunga kingine

Wanajeshi na wafanyakazi wakitengeneza uzio kukabiliana na dhoruba jingine

Wananchi wakiwa wamejipanga kupokea msaada

Wavuvi wa Vietnam wakiziweka sawa boti zao


























No comments:
Post a Comment