HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » NATIONAL GEOGRAPHIC WASHINGTON, DC YAFAGILIA MBUGA ZA WANYAMA ZA TANZANIA

National Geographic ya Washington, DC siku ya Jumatano, Dec 11, 2913 walionyesha vivutio mbalimbali vilivyopo kwenye mbuga zetu za wanyama kwa wahudhuriaji ambao wengi wao walikua Wamarekani pia ulialikwa Ubalozi wa Tanzania akiwemo Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknologia, Mhe. January Makamba,
Mhe. January Makamba akitoa shukurani zake kwa Nafional Geographic kwa jitihada zao za kusaidia kutangaza hifadhi za Taifa za wanyama pori

ENDELEA KUTIZAMA TUKO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI


Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akiwapongeza National Geographic kwa kuwa Mabalozi wa Tanzania nchini Marekani na kuahidi kufanya nao kazi kwa karibu zaidi na mlango wa Ubalozi wa Tanzania upo wazi pindi wanapohitaji msaada.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania National Parks, Bwn. Allan Kijazi nae akiwapongeza National Geographic kwa jitihada zao za kutangaza mbuga za wanyama pia aliwahakikishia wahudhuriaji Tanzania ndio mahali pekee kwenye vivutio na aina nyingi ya wanyama hao.
Andrew Evans mfanyakazi wa National Geographic ambaye ndiye aliyetembelea mbuh=ga za wanyama Tanzania, akiwaonyesha wahudhuriaji picha mbalimbali za wanyama na kuwaelezea kuhusu Tanzania kwamba ni nchi ya Amani na Utulivu na Watanzania waliojaa na upendo kwa kila mtu.

Akianza kuelezea alianza kuwaonyesha Khanga kwamba hutumika kwenye shughuli nyingi na kwamba utaiona kila pahala,
Pia alionyesha picha ya kukutana na marafiki zake hao kwenye picha na yeye alipewa jina la Mzungu, Andrew Evans anaufahamu mkubwa wa hifadhi za Taifa jinsi alivyozielezea na vitu vilivyomo lazima uatatamani kuelekea huko kesho.
Mhe. January Makamba akimpongeza Andrew Evans kwa jinsi anavyoitangaza Tanzania.
Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mhe. January Makamba wakiongea na wahudhuriaji walijaribu kudadisi mambo mengine kutoka Tanzania na kuahidi kuja nchini Tanzania kutembelea mbuga za wanyama.
Mhe. January Makmba akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula ndani ya thieta za National Geographic, Washington, DC.
Kutoka kushoto mstari wa mbele ni Afisa wa Ubalozi Mindi Kasiga, Mkurugenzi mkuu wa Tanzania National Parks, Bwn. Allan Kijazi, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknologia, Mhe. January Makamba na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na wahudhuriaji wengine waliofika National Geographic ya Washington, DC. Picha kwa hisani ya Vijimambo Blog

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: