Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu, Joseph Warioba, akimkabidhi
Rais Jakaya Kikwete, rasimu ya pili ya Katiba mpya, leo kwenye Viwanja vya Karimjee jijini, Dar es Salaam, baada ya kumalizika kwa kazi ya kukusanya maoni ya wananchi.
Jaji Warioba akikabidhi rasimu hiyo pia kwa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Rais Jakaya Kikwete akiwakabidhi Rasimu ya Katiba Spika wa Baraza la
Wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho (kulia), Rais mstaafu wa Awamu
ya Pili, Ali Hassan Mwinyi (katikati) na Waziri Mkuu wa zamani, Cleopa
Msuya (kushoto) baada ya kukabidhiwa rasmi na Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba, Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi Rasimu ya Katiba Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
Baadhi ya viongozi wa vyama wakiwa katika hafla hiyo.
Baadhi ya viongozi wastaafu na waasisi wa Tanzania, wakiwa wameshikilia rasimu
hiyo, baada ya kukabidhiwa na Rais Jakaya Kikwete jana. Kutoka kushoto
ni Balozi mstaafu Job Lusinde, Sir George Kahama, Hassan Nassor Moyo na
Jaji mstaafu, Mark Bomani na aliyekuwa Mkuu wa Majeshi, Mirisho
Sarakikya
Baadhi ya wananchi na wanazuoni wakiwa katika hafla hiyo ya kukabidhiwa
Rais Jakaya Kikwete na Dk. Ali Mohamed Shein, rasimu ya mwisho ya
katiba.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali wakiwapongeza wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya katiba baada ya makabidhiano ya Rasimu ya pili ya Katika katika viwanja vya Karimjee Hall jijini Dar es salaam
Rais Jakaya Kikwete akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia.
Rais Jakaya Kikwete, Dk. Shein, Dk. Bilal, Maalim Seif Sharif Mahad na viongozi wengine wakiwa na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba










No comments:
Post a Comment