HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » UTAFITI: DAWA LA KULAINISHA NYWELE CHANZO CHA UVIMBE TUMBONI, KUBALEHE KABLA YA WAKATI


Utafiti umebaini kuwa matumizi ya dawa za kulainisha nywele 'relaxer’ ni chanzo cha wanawake kuota uvimbe kwenye kizazi unaojulikana kitaalamu kama ‘fibroids’.
 
Kadhalika kuweka dawa hizo kwenye nywele kunasababisha mabinti kuvunja ungo wakiwa na umri mdogo.
Utafiti huo ulifanywa hivi karibuni na kuchapishwa na Jarida la Marekani la Magonjwa ya Binadamu.
 
Jarida hilo la Annals of Epidemiology-Journal, limeandika kuwa wanasayansi waliwachunguza wanawake Wamarekani weusi kuanzia mwaka 1997 hadi 2009 na kubaini kuwa kuna viwango vya zaidi ya mara tatu vya kuota uvimbe wa kizazi kwa wanawake weusi kunakotokana na dawa za ‘relaxer’ ikilinganishwa na wanawake wengine.
 
Walibaini kuwa uvimbe huo unahusishwa na  matumizi ya kemikali za nywele za ‘relaxer’ na viambata vyake ambavyo huingia mwilini kupitia ngozi ya kichwa iliyojeruhiwa kwa michubuko na kuunguzwa  na dawa.
 

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINIJarida liliripoti kuwa Waamerika weusi wanapata hedhi kabla ya kufikia miaka 10 pia walibainika kukumbwa na ‘fibroids’ na kuanza kupata siku zao za mwezi  wakiwa wadogo kuliko ilivyotakiwa kutokana na dawa hizo.
 
Wanawake 300 wakiwamo Wamarekani weusi na weupe,  wengine wa asili ya Caribbean na Hispania waishio  jijini New York walichunguzwa katika utafiti huo.
 
Matokeo yalibainisha kuwa licha ya wanawake kupata hedhi wakiwa na umri kati ya miaka nane hadi 19 lakini kwa upande wa Waamerika weusi wamegundulika kuwa wanawahi kupata hedhi kuliko watu wa rangi nyeupe kutokana na kutumia ‘relaxer’ na viambata vyake.
 
Viambata hivi ni kama mafuta ya nywele, dawa za 'steaming', ‘spray’ losheni na ‘conditioner.’
 
Kinachoonekana katika utafiti huo ni uhusiano baina ya ‘relaxer’ na kuwepo uvimbe wa aina za ‘fibroid’ na `tumour’ na  mabinti kupevuka mapema lakini hakuna maelezo ya usababishaji wa magonjwa na hali hiyo.
 
Kufuatia maelezo hayo wataalamu wanakosoa kuwa sekta ya urembo na vipodozi vya nywele haidhibitiwi na Mamlaka ya Marekani ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (FDA).
 
Wanaeleza kuwa hakuna utaratibu maalumu wa kufuatilia na kufahamu jinsi kemikali za kutengeneza dawa na vipodozi vya nywele za watu weusi zilivyo na madhara yake.
 
FIBROID
Unaoota ndani ya kizazi, mara nyingi hauna seli za saratani na wataalamu wamegundua kuwa unaota kutokana na nyuzi za misuli ya mwili.
 
Fibroid zina sura ya mapafu ya mnyama ni nyama laini zinapoota huanza na ukubwa wa njegere lakini hukua na kuongezeka  hadi kimo cha tikitimaji.
 
Katika taarifa hiyo ya relaxer iliyoko kwenye mtandao, baadhi ya walioijadili walipendekeza kufanyike utafiti zaidi wa madhara yake kwa watumiaji. Walisema nywele za asili ni bora na zinalinda afya na uzuri wa mtu bila kutumia dawa.
 
Muuguzi Deborah Jones wa Virginia, Marekani, anasema madaktari wengi wamewaasa watu kuachana na matumizi ya kemikali kama relaxer ili kuepuka uwezekano wa kupata maradhi ya saratani. 
 
“Wengi wanadhani kuwa nywele za kipilipili ni vigumu kuzitunza na zinapoteza muda kuzishughulikia , lakini kama utatumia zaidi ya saa mbili saluni ili kuwekewa relaxer, kukausha , kusetiwa kama ungekuwa na kipipili usingepoteza muda mwingi kiasi hicho.”
 
Ni bora kama madaktari watawahimiza watu kuachana na kemikali hizi za relaxer na dawa za kubadilisha rangi ambazo lengo lake ni kulazimisha watu kutumia fedha nyingi kwenye vipodozi badala ya mambo muhimu ya maisha. 
 
WATANZANIA
Kwa Watanzania ni wakati wa  wanawake kujihoji  hasa wale wanaotumia relaxer muda wote,  wakiwa wajawazito, wakinyonyesha na pia huwapaka mabinti zao.
 
Mamlaka ya Chakula na  Dawa (TFDA) na  Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali  wachunguze vipodozi vya nywele ambavyo kama ilivyo kwa Marekani  yapo maelezo kuwa havidhibitiwi na  mamlaka ya dawa ya FDA.
Imetafsiriwa kutoka kwenye mtandano  na Gaudensia Mngumi 
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: