Kuna lori lililokuwa limebeba kontena limejaribu kupita daraja
linalounganisha Ukonga
(Banana)- Tabata Segerea- Kinyerezi na Mbezi
limeharibika kabisa kwa kutumbukia na lori , kwa sasa foleni ni kubwa
magari yote yanarudi, kwa wanaotoka mjini ni vyema kutumia njia ya Vingunguti kupitia Barakuda
kwenda Segerea, Kinyerezi na Mbezi kwani daraja limearibika sana.
NI VYEMA SHERIA IKACHUKUA MKONDO WAKE, haiingi akilini mjinga mmoja kukata mawasilino wa watu wote kwenye njia muhimu kama hii. Mfumo wa kudhibiti malori ya mizigo ni dhaifu sana nchini, madereva
wangepewa route za kupita pale wanapotoa mizigo bandari na wanapoingiza
mizigo hapa mjini kutoka mikoani wahusika mmeliona hili mpaka linatokea yametokea mangapi. Daraja hili mwisho ni tani 10 kuna vibao vimeandikwa kabisa lakini kunafanyika mambo kama haya.
No comments:
Post a Comment