HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » UBALOZI WA AFRIKA YA KUSINI NA UMOJA WA MATAIFA (UN) WAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA NELSON MANDELA

002
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Joyce Mends-Cole akizungumza na baadhi ya wadau waliohudhuria katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Nelson Mandela kabla ya kusoma ujumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Mooniliyofanyika leo duniani kote na hapa nchini imeadhimishwa katika shule ya watoto wenye mahitaji maalum na kudhaminiwa na Vodacom.
DSC_0547
Kaimu balozi wa Afrika Kusini nchini, Bw. Terry Govender akitoa shukrani kwa wadau waliojumuika pamoja na Ubalozi huo kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela yaliyofanyika leo jijini Dar katika shule ya Watoto Wenye Mahitaji Maalumu Sinza Mapambano.

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI


Na Mwandishi wetu
Wafanyakazi wa Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini Tanzania, Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania leo Julai 18, 2014 wameungana na taasisi na wananchi kutoka sehemu mbalimbali duniani katika kuadhimisha siku ya Kimataifa ya aliyekuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini aliyejitolea maisha yake kupigania na kuondoa vitendo vya ubaguzi wa rangi na unyanyasaji nchini humo, hayati Nelson Mandela.
Siku ya Mandela ilitangazwa na Umoja wa Mataifa kuadhimishwa tarehe ya leo kila mwaka na imekuwa ikiadhimishwa siku kama hii sehemu mbalimbali duniani ambapo taasisi mbalimbali hushiriki kufanya kazi za kujitolea kuhudumia jamii kwa muda wa dakika 67 kumuenzi kiongozi huyu aliyeleta mapinduzi makubwa yenye historia ya kipekee duniani.
Katika kuienzi siku hii ya leo,Ubalozi wa Afrika Kusini nchini ,Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), wafanyakazi wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom wameshiriki katika shughuli za kuhudumia jamii ambapo wamesafisha mazingira ya shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Sinza jijini Dar es Salaam ambapo pia wamegawa zawadi mbalimbali kwa watoto wanaosoma shuleni hapo.
Kaimu balozi wa Afrika kusini nchini, Terry Govender alisema wanajivunia kuwa na kiongozi hodari kama Nelson Mandela ambaye alijitolea nusu ya maisha yake kupigana dhidi ya ubaguzi nchini Afrika Kusini na kuwaasa watu kufwata nyayo zake kwani ni mfano wa kuigwa duniani.
“Kama ilivyokuwa kwa Nelson Mandela, alitumia muda wake na nguvu zake kuhamasisha amani na usawa na kupigania haki za wanyonge, Mandela pia kupitia mfuko wa watoto aliouanzisha, aliamini kuwa watoto wote wanapaswa kufurahia kwa kutokuwepo kwa njaa, unyonyaji, unyanyasaji na kutokuwa na makazi, hivyo ndio maana sisi tunashiriki kwa kuirudishia jamii kile tulichonacho na kufurahi pamoja na hawa watoto”, alisema.
Akiongea juu ya kushiriki katika tukio hili muhimu, Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu alisema kuwa kampuni inaona fahari kubwa kushiriki na kutoa baadhi vifaa muhimu katika siku ya kiongozi mashuhuri duniani mwenye historia ya pekee katika mapambano ya kutokomeza vitendo vya kufifisha haki za binadamu.
“Vodacom tunajivunia kushiriki katika shughuli za kijamii za kuadhimisha siku maalum ya kiongozi shupavu wa Afrika,hayati Nelson Mandela, aliyejitolea maisha yake yote kupambana na vitendo vya ubaguzi wa rangi nchini Afrika na kuhakikisha vinatokomezwa kwa njia ya amani”alisema Nkurlu.
DSC_0522
Mwalimu Mkuu wa shule ya Watoto Wenye Mahitaji Maalumu Sinza Mapambano, Simon Milobo akizungumza na baadhi ya wageni waalikwa waliofika shuleni hapo kutumia muda wao wa dakika 67 kufanya kazi za kijamii za kujitolea katika shule hiyo, kama usafi wa mazingira yanayoizunguka shule, kupaka rangi baadhi ya madarasa, kupika, michezo mbalimbali na watoto hao kuonyesha vipaji mbalimbali walivyonavyo vikihusishwa na namna Nelson Mandela alivyokuwa akiwathamini na kuwapenda watoto.
Alisema mbali na kumuenzi hayati Mandela kwa kutokomeza vitendo vya ubaguzi,Vodacom inatambua mchango mkubwa wa kiongozi huyo alivyokuwa mstari wa mbele kuhudumia jamii na moja ya sera ya kampuni ya Vodacom ni kushiriki katika kazi za kuhudumia jamii.
“Kwetu Vodacom kushiriki katika shughuli za kijamii ni moja ya sera yetu hivyo siku hii ni muhimu kwetu kama kampuni na wafanyakazi wake wote na siku zote tutakuwa mstari wa mbele kushiriki na kusaidia katika shughuli za jamii.Alisema.
Hayati Nelson Mandela ambaye alifariki mwaka jana Desemba atakumbukwa daima kwa ushupavu wake wa kutokemeza vitendo vya kibaguzi nchini Afrika ya Kusini na baada ya kustaafu aliendelea kuisaidia changamoto mbalimbali za kijamii kupitia taasisi ya Mandela Foundation.
DSC_0575
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar, Ramadhani Madabida akizungumza neno wakati wa maadhimisho hayo.
DSC_0478
Afisa Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Gloria Mtui akigawa T-shirt za Vodacom meza kuu kwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Joyce Mends-Cole (mwenye kofia ya blue).
001
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (Kushoto)pamoja na Afisa wa Ubalozi wa Afrika ya Kusini Nkhetheleni Mphohoni na Afisa Mawasiliano wa Vodacom, Gloria Mtui wakigawa zawadi za tisheti na kofia kwa wanafunzi na wa shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Sinza jijini Dar es Salam wakati wa maadhimisho ya siku ya Mandela iliyoandaliwa na Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini na kufanyika leo shuleni hapo.
DSC_0501
Baadhi ya wadau kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa, Makampuni mbalimbali na Taasisi walioshiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya Mandela kwenye shule ya Watoto wenye Mahitaji Maalum, Sinza Mapambano.
DSC_0562
DSC_0558
Baadhi ya wanafunzi wa wanaosoma katika shule yenye mahitaji maalum ya Sinza jijini Dar es Salam,wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Nelson Mandela iliyoandaliwa na Ubalozi wa Afrika ya Kusini nchini kwa ushirikiano na Vodacom Tanzania.
003
Afisa Habari wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC), Stella Vuzo, (kulia) akibadilishana mawazo na maofisa wa kampuni ya Vodacom, Matina Nkurlu na Gloria Mtui, kushoto ni Afisa wa Ubalozi wa Afrika ya Kusini Nkhetheleni Mphohoni ,wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Nelson Mandela iliyofanyika leo duniani kote na hapa nchini iliyoandaliwa na Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini na kuadhimishwa katika shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Sinza jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
DSC_0633
Pichani ni baadhi ya wadau wakiwapaka rangi Watoto wa shule msingi wenye Mahitaji Maalum wa Shule Sinza Mapambano wakati wa maadhimisho hayo.
DSC_0642
Mmoja wa watoto anayesoma kwenye shule hiyo akitazama taswira mbalimbali kwenye simu ya mmoja wa wadau waliojumuika kufurahi pamoja na watoto hao kwenye maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.
DSC_0629
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu akishirikiana na mmoja wa watoto wa shule hiyo kukata nyasi kwenye mazingira ya shule hiyo.
DSC_0646
DSC_0661
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Joyce Mends-Cole akishiriki kufanya usafi na baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Mandela inayoadhimishwa kila mwaka Julai 18 duniani kote.
005
Afisa Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Gloria Mtui akishikiana na wanafunzi wanaosoma katika shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Sinza jijini Dar es Salam,kusafisha mazingira ya shule hiyo wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Mandela iliyoandaliwa na Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini kwa ushirikiano wa Vodacom.
DSC_0722
Baadhi ya vijana kutoka katika kikundi cha WAKALI JOGGER wakishiriki zoezi la kusafisha mtaro ulio nje ya uzio wa shule ya Watoto wenye Mahitaji Maalum Sinza Mapambano jijini Dar.
DSC_0735
Mdau Lauren Kiiza kutoka UNIC akishiriki kusafisha mtaro wa shule Watoto wenye Mahitaji Maalum Sinza Mapambano wakati wa maadhimisho Siku Mandela Duniani iliyoadhimishwa duniani kote leo.
DSC_0454
DSC_0484
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa Bi. Usia Nkhoma Ledama akipiga picha kwenye bango la maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: