CHADEMA YAKANUSHA HABARI ZA KUHUSIKA NA KIFO CHA MWANGOSI

 Mkurugenzi  wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, John Mnyika, akizungumza na waandishi wa habari.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekana shutuma zilizoelekezewa kwao kuwa wanahusika na kifo cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi.Baadhi ya viongozi wa Chadema kutoka kushoto ni Ofisa Habari, Tumaini Makene, Mbunge wa Ubungo Mh. John Mnyika, Ofisa Mwandamizi Mafunzo na Uendeshaji, Mohamed Mtoi, na mwenye gwanda ni Katibu Mtendaji, Ofisi ya Katibu Mkuu, Victor Kimesera.
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, Mhe. John Mnyika, ameeleza kuwa hawahusiki na mauaji hayo bali ni propaganda zinazoenezwa ili kuwasahaulisha wananchi juu ya suala la katiba linaloendelea.
Waandishi wa habari wakifuatilia taarifa ya Chadema.
Mnyika alieleza kuwa wanaoeneza habari hizo ni wale ambao wanataka kuizuia Chadema na Ukawa kwa ujumla kuendelea na harakati za kupigania katiba ya wananchi ikiwemo kufanyika maandamano ya kitaifa iwapo Rais Kikwete hataingilia kati kulisimamisha zoezi la katiba mpya.

No comments

Powered by Blogger.