POLISI WAPORWA BUNDUKI JANA MKOANI TANGA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Muonekano wa askari hao baada ya kuvamia na kuwajeruhi siku ya jana Tanga.
Watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, wamewavamia na kuwajeruhi askari mwenye no G369 PC Mansour na Hv507 PC Mwalimu, wakiwa doria ya pikipiki ambao walinyang'anywa silaha mbili aina ya SMG no 14301230 na 14303545 na watu wasio julikana mkoani Tanga.
Mchoro wa ramani unaoonyesha matokeo ya Barabara Tanga.
Taarifa ya Jeshi hilo kwa vyombo vya habari imesema tukio hilo limetokea Januari 26, 2015 majira ya saa 23:30hrs eneo la barabara 04 jijini humo.

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

Aidha, imesema mmoja wa majeuhi askari mmoja no H 507 PC Mansour amejeruhiwa vibaya maeneo mbalimbali ya mwili na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa Bombo.
Katika uchunguzi wa awali Polisi wamefanikiwa kumtia hatia hatiani mtuhumiwa mmoja, Ayubu Haule, (27), fundi Radio Mkazi wa Corner Z Amboni Kiomoni ambaye alikamatwa eneo la tukio akijaribu kutoroka na pikipiki na mara baada ya kupekuliwa ndipo alipokutwa na mchoro wa ramani unaoonyesha matokeo ya Barabara na kufunguliwa kesi yenye no TAN/IR/322/2015.
Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na Jeshi hilo huku timu ya Intel na makachero wa Polisi ikiendelea kufanya doria pamoja na Section 2 za FFU.

CHANZO: JAMII FORUMS

No comments

Powered by Blogger.