MKUU WA MKOA WA MTWARA MH. HALIMA DENDEGU AZINDUA RASMI SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2016 KATIKA UWANJA WA MASHUJAA.

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh. Halima Dendegu akitoa Hotuba yake kwa wakazi wa Mtwara na Kuzindua Rasmi Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2016 linaloendeshwa na Shirika la Kimataifa la  OXFAM Tanzania
 Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mh. Fatma Ally akizungumza na wakazi wa Mtwara,wageni mbalimbali na wadau pia kufungua rasmi sherehe hizo wakati wa Maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani na Uzinduzi wa Shindano la Mama wa Chakula kwa Mwaka 2016
 Meneja wa Programu ya Uwazi na Utawala Bora kutoka Shirika la Kimataifa la OXFAM Bi. Betty Mlaki akitoa salamu za shukurani kwa niaba ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika Hilo Jane Foster wakati wa Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani na uzinduzi rasmi wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula 2016
 Kamanda Mkuu wa Polisi Mkoa wa Lindi Renatha Mzinga akizungumzia nafasi ya Mwanamke katika kujenga Taifa wakati wa siku ya Maadhimisho ya Sikukuu ya wanawake Duniani.
 Kamishna Msaidizi wa Polisi Tatu Abdallah Mfaume ambaye ni Mkuu wa Dawati la Jinsia na Ulinzi wa Mtoto kutoka Makao Makuu ya Polisi Dar es salaam, akizungumzia juu ya Dawati la Jinsia linavyofanya kazi
 Mshereheshaji akiendelea na kutoa Utaratibu 
Mwanamuziki wa Muziki wa Kizazi Kipya Mwasiti akitumbuiza wakati wa Sherehe za Siku  ya Mwanamke Duniani
 Bi. Jovitha Mlay Kutoka Shirika la Kimatafa la OXFAM Tanzania akizungumza na wakazi wa Mtwara juu ya wanawake na uziduaji
 Bw.  Mohammed Mapalala kutoka Morogoro anayehusika na Maswala ya Ardhi akizungumzia juu ya Haki ya Ardhi kwa wanawake
 Meneja wa Utetezi Kutoka Shirika la OXFAM Tanzania Bi. Eluka Kibona akitoa Maelezo ya  kina kuhusu Shindano la Mama Shujaa wa Chakula ambapo Msimu huu wa Tano linatarajiwa kuanzi mwezi Septemba na kurushwa katika Runinga ya ITV 
Mwanamuziki Vitaris Maembe akitoa Burudani ya Nguvu wakati wa Sherehe ya Siku ya Wanawake Duniani na Uzinduzi Rasmi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh. Halima Dendegu akitembelea katika Mabanda mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani a Uzinduzi Rasmi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula kwa Mwaka 2016
Mwanamuziki matata wa Miondoko ya Taarabu Jike la Simba Bi. Aisha Mashauzi akitoa Bonge la Burudani wakati wa kilele cha Siku ya wanawake Duniani
Burudani ikiendelea
Mamia ya wakazi wa Mtwara wakiwa katika Sherehe ya Siku ya Wanawake Duniani na uzinduzi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula kwa mwaka 2016, katika Uwanja wa Mashujaa.

No comments

Powered by Blogger.