HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » SUMATRA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI MADEREVA NA MAKONDAKTA WOTE WATAKAOWATOZA ABIRIA NAULI KUBWA TOFAUTI NA ZILIZOPANGWA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi Usafiri wa Majini na Nchi Kavu  (SUMATRA) Mkoa wa Kilimanjaro  kuwafikisha mahakamani madereva wote na makondakta wanaowatoza abiria nauli kubwa tofauti na zilizopangwa na ofisi hiyo.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Afisa Mfawidhi Bw.Tadei Mwita alipokuwa akijibu kero ya mkazi wa mkoa huo kwa njia ya simu iliyotolewa na Gazeti  la Mwananchi Machi 04, mwaka huu,iliyozungumzia  daladala zinazofanya safari zake kati ya Moshi Mjini - Himo kuwatoza nauli ya shillingi 1000 abiria wanaoshuka maeneo ya Kiboriloni, Sango Pumuani na Kawawa road tofauti na nauli iliyopangwa na SUMATRA katika vituo hivyo.  

“Kuanzia wiki ijayo wadau wote  watakao kuja kuomba leseni kwa ajili ya usafirishaji wa abiria ndani ya mkoa huu watahitajika kuonyesha nauli watakazo toza abiria katika vituo vya katikati kabla ya kufika kituo cha mwisho cha safari zao,”alisema Bw.Mwita.

 Bw.Mwita alisema hivi sasa SUMATRA Mkoa wa Kilimanjaro  imeanzisha utaratibu wa kuwataka wadau wote wanaotarajia kuanza kutoa huduma za usafiri wa daladala mkoani hapo kuonyesha nauli watakazo toza katika  vituo vya katikati kabla ya kufika kituo cha mwisho.

 Hata  hivyo Afisa huyo aliwashauri wakazi wa maeneo kama kiboriloni kwa sasa kupanda daladala za Kiboriloni kwa kuwa zipo nyingi ili kuepuka usumbufu unaojitokeza.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: