HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA MAKATIBU TAWALA WAPYA WA MIKOA 10 IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Ndugu Jumanne Abdallah Sagini kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Ndugu Selestine Muhochi Gesimba kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Ndugu Amantius Casmiri Msole kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Ndugu Zuberi Mhina Samataba kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Thea Medard Ntara kuwa katibu Tawala wa mkoa wa Tabora, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Ndugu Richard Nkingwa Kwitega kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Eng. Aisha Salim Amour kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Kilimanjaro, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Eng. Zena Ahmed Said kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Tanga, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Ndugu Albert Gabriel Msovela kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Angelina Mageni Lutambi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Tawala wapya wa Mikoa 10 mara baada ya Kuwaapisha. Kulia kwake ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Kushoto kwake ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makatibu Tawala wapya mara baada ya kupiga nao picha ya pamoja Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Eng. John Kijazi.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Eng. John Kijazi mara baada ya kumaliza kuwaapisha Makatibu Tawala wa mikoa 10 Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Makatibu Tawala wapya kumi aliowateua tarehe 25 Aprili, 2016 na kuwapangia vituo vyao vya kazi.
Makatibu Tawala hao wameapishwa leo tarehe 27 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam na kisha wametia saini hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi lililoendeshwa na Kamishna wa maadili Sekreatieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mheshimiwa Jaji Salome Kaganda na kushuhudiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Makatibu Tawala walioapishwa ni;

1. Arusha - Richard Kwitega
2. Geita -  Selestine Muhochi Gesimba
3. Kagera -  Armatus C. Msole
4. Kilimanjaro - Eng. Aisha Amour
5. Pwani -  Zuberi Mhina Samataba
6. Shinyanga -  Albert Gabriel Msovela
7. Singida - Dr. Angelina Mageni Lutambi
8. Simiyu - Jumanne Abdallah Sagini
9. Tabora - Dkt. Thea Medard Ntara
10. Tanga - Eng. Zena Said
Makatibu Tawala wengine wa Mikoa ambao hawakuapishwa leo, ni wale waliohamishwa vituo vya kazi na wale waliobaki katika vituo vya kazi walivyokuwep,o ambao tayari walishakula kiapo cha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
27 Aprili, 2016

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: