HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » MSANII SNURA APIGWA STOP KUJIHUSISHA NA MUZIKI NA NYIMBO YAKE YA CHURA YAFUNGIWA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza kuufungia wimbo na video ya Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Snura Mushi unafahamika kwa jina la CHURA kutokana na kutokuwa na maadili ya Mtanzania.

Wimbo huo pia umezuiwa kutumbuizwa mahala popote na kufungiwa kuchezwa kwenye redio na runinga nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo, Zawadi Msalla, amewaonya watu kutousambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp na Istagram na kuongeza kuwa wale watakaokiuka agizo hilo watashtakiwa kwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.

Pia Wizara hiyo, imesitisha maonyesho yote ya hadhara ya Msanii huyo, mpaka pale atakapo kamilisha taratibu za usajili wa kazi zake zote kwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Serikali imewataka wanasii mbali mbali nchini, kujiuliza mara mbili kabla ya kubuni kazi zao za sanaa.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: