HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » Maombi ya wabunge waliofukuzwa CUF yasikilizwa

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam hivi sasa inaendelea na usikilizwaji wa maombi ya wabunge waliofukuzwa na Chama cha Wananchi (CUF), ya kutaka kusimamishwa kuapishwa kwa wabunge wapya walioteuliwa juzi kuziba nafasi zao.
Hata hivyo, badala ya kusikiliza maombi ya msingi, mahakama inasikiliza mapingamizj ya awali yaliyowasilishwa na jopo la Mawakili wa Serikali kwa niaba ya wajibu maombi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na Katibu wa Bunge pamoja na pingamizi lililowasilishwa na Bodi ya Wadhamini CUF, na wabunge wateule.
Waombaji katika maombi haya wanawakilishwa na mawakili wawili, Peter Kibatala na Omari Msemo, wakati NEC na Bunge wanawakilishwa na jopo la mawakili nane wa Serikali wakiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Gabriel Malata, wakati Bodi ya Cuf na wabunge wateule wanawakilishwa na Wakili Mashaka Ngole.
Baada ya kumaliza hoja zao za pingamizi, Kibatala na Msemo watajibu hoja hizo na baadaye Jaji Lugano Mwandambo atatoa uamuzi ama leo hii au siku nyingine atakayopanga.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: