HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » Waliokamatwa na mzigo wa almasi JNIA wafikishwa Mahakamani Kisutu

Baada ya Serikali kuanza kuwashughulikia wale wote wanaohujumu uchumi wa nchi na kuiibia nchi rasilimali zake, watuhumiwa waliokamatwa na mzigo wa Almasi zenye thamani ya shilingi bilioni 32.3 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wamefikishwa katika Mahakama ya Kisutu leo asubuhi Septemba 15.

Mzigo huo wa Almasi uliokuwa unatoka mgodi wa Mwadui ulizuiliwa na Serikali kwa lengo la kuufanyia tathmini upya ili kujua thamani halisi baada ya thamani iliyokuwa imetajwa awali kutiliwa mashaka na Serikali.

Baada ya kubainika kuwa wahusika walidanganya thamani, Jeshi la Polisi liliwashikilia watuhumiwa wanne huku uchunguzi na hatua nyingine za kisheria zikifuatwa baada ya kuzuiwa kwa mzigo huo.

Mgodi wa Mwadui unamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali na Kampuni ya Petra Diamonds ya Afrika Kusini ambapo Serikali ina hisa 25% na Petra Diamonds ina hisa 75%.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: