Tanzania yashukuru China, UNESCO ufadhili sekta ya elimu ya ufundi


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof William Anangisye akitoa hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Carolyne Nombo wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Michel Toto akitoa neon la ukaribisho wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Picha juu na chini ni Balozi wa China nchini,Chen Mingjian akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Baadhi ya wanafunzi kutoka tasisi mbalimbali za vyuo vya elimu ya juu, waratibu wa taasisi za elimu ya juu, wataalamu kutoka vyuo vya elimu ya ufundi kutoka nchi 6 zilizoshiriki ikiwemo Tanzania, wadau wa sekta binafsi pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa UNESCO walioshiriki ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Mkuu wa Kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu , Sayansi na utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Faith Shayo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Mratibu wa mradi wa CFIT III kutoka makao makuu ya Shirika la UNESCO nchini Ufaransa, Bi. Qinglin Kong akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Mgeni rasmi na meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi kutoka tasisi mbalimbali za vyuo vya elimu ya juu, waratibu wa taasisi za elimu ya juu, wataalamu kutoka vyuo vya elimu ya ufundi kutoka nchi 6 zilizoshiriki ikiwemo Tanzania, wadau wa sekta binafsi pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa UNESCO walioshiriki ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Mgeni rasmi na meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi kutoka tasisi mbalimbali za vyuo vya elimu ya juu nchini walioshiriki ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Picha ya pamoja wa washiriki kutoka nchi 6 zinazonufaika na mradi CFIT III ikiwemo Tanzania, waratibu wa kutoka taasisi za elimu ya juu, wataalamu kutoka vyuo vya elimu ya ufundi pamoja na wafanyakazi wa UNESCO wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu (CFIT III) unaoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa na serikali ya watu wa China uliofanyika katika ukumbi wa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).


Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Tanzania imeishukuru Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na UNESCO kwa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya elimu ya juu ya ufundi barani Afrika kwa lengo la kujenga nguvu kazi ya kiufundi na bunifu kwa maendeleo ya mataifa hayo.

Kauli imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Carolyne Nombo katika hotuba yake iliyosomwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof William Anangisye akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa mradi wa kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu katika kuendeleza ufundishaji unaozingatia soko la ajira na ujifunzaji CFIT awamu ya tatu.

Mradi huo unaotambulika kama China Fund In Trust Project Phase III (CFTI-III) unaendeshwa katika nchi sita ikiwamo Tanzania. Nchi nyingine ni Côte d’Ivoire, Ethiopia, Gabon, Senegal na Uganda.

Mradi huo ambao pia unalenga kuimarisha uhusiano kati ya vyuo vikuu na viwanda unatekelezwa kwa muda wa miaka 4 kwa bajeti ya Dola za Marekani milioni 7.5.

Nombo alisema kutokana na mradi huo vyuo vikuu vimeanza kuwa na rasilimali watu bora pamoja na miundo mbinu ya kufundishia na utafiti ili kuweza kutoa elimu stahiki ya kiufundi kwa vijana ili kufikia hitaji halisi la soko.

Alisema kupitia mradi huo mataifa yameweza kubadilika na kukabiliana na uhaba wa wanafunzi wanaochukua masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati

Pia amesema kwamba ni mtarajio yake kwamba China kupitia Unesco wataendelea kusimamia mradi huo kwa miaka mingine ili kuweza kuhakikisha kwamba mitaala inaboreka  na vijana wanaotoka wanakidhi haja ya soko la ajira.

Naye Balozi wa China nchini,Chen Mingjian pamoja na kuipongeza Tanzania kwa kukubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo mkubwa wa mwaka, alisema  amefurahishwa kuona kwamba Mpango Kazi wa Ushirikiano wa China na Afrika wa Dakar (2022-2024), Awamu ya Tatu ya Mfuko wa Ufadhili wa UNESCO-China umekuwa na mafanikio makubwa.

Alisema kutokana na mafanikio hayo serikali yake itaendelea kutekeleza mradi huo na utazingatia haya ya kuuendeleza kwa miaka mingine minne yaani kuanzia mwaka huu hadi mwaka 2026.

"Kwa kutoa ufadhili huu, China inasaidia kukuza maendeleo ya teknolojia ya habari na kuboresha uwezo na kiwango cha mafunzo kwa taasisi za elimu na wafanyakazi katika nchi za Afrika. " alisema balozi huyo na kuongeza kuwa China iko tayari kufanya kazi na pande zote kutekeleza Mpango Kazi wa Dakar, kuimarisha ushirikiano wa elimu, na kuchangia katika kukuza maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya nchi zote na kujenga jumuiya ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja katika enzi mpya.

China ni mojawapo ya vyanzo vikubwa zaidi vya ufadhili vya kiserikali vya UNESCO vinavyoorodheshwa mara kwa mara kati ya wafadhili wakuu 20 wanaotoa michango ya hiari, na mchangiaji mkubwa zaidi wa michango iliyotathminiwa kwenye bajeti ya kawaida ya UNESCO.

Madhumuni ya jumla ya CFIT III ni kuongeza uwezo wa taasisi za elimu ya juu ili kukabiliana na mahitaji ya ujuzi kwa maendeleo ya taifa kwa kuwezesha ushirikiano kati ya taasisi za elimu ya juu na sekta, kuimarisha ufundishaji unaozingatia soko la ajira, na kuimarisha ujifunzaji unaozingatia uwezo.

Naye Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu , Sayansi na utamaduni (UNESCO) nchini, Michel Toto  akikaribisha washiriki wa kongamano hilo la siku tatu, alitoa shukurani kwa serikali ya China  kwa kutoa fedha zinazowezesha kuleta mabadiliko katika elimu barani Afrika.

Pia aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hususan Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa msaada wake thabiti na kujitolea kwa Mradi wa CFIT III ili kukuza elimu ya ufundi stadi.

"Ni kupitia maono ya uongozi wa Wizara, tumeanzisha ushirikiano imara, kukusanya rasilimali kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa Mradi wa CFIT III nchini Tanzania." alisema Toto.

Alisema UNESCO wamefurahishwa na mtazamo na dhamira ya Serikali kuchagiza Maboresho ya Sekta ya Elimu yanayoendelea ambayo yatapatanisha na viwango vya kimataifa na mazoea bora.

Alisema mradi wa CFIT III unakamilisha kikamilifu mageuzi ya elimu yanayofanyika Tanzania ili kuendeleza Ajenda ya Elimu 2030.

"Kupitia mradi wa CFIT III, tunakuza ushirikiano kati ya taasisi za elimu ya juu na sekta hiyo, kukuza mbinu za ufundishaji zenye mwelekeo wa soko la ajira, na kuimarisha ujifunzaji unaozingatia uwezo. Hii huwapa wanafunzi ujuzi na maarifa yanayohitajika kwa soko la ajira na mahitaji ya jamii yanayoendelea" alisema Toto

Nchini Tanzania, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) ni wanufaika wa moja kwa moja wa Mradi wa CFIT III.

No comments

Powered by Blogger.