HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » KITUO CHA AFYA HIMO JIMBO LA VUNJO CHAPATA VIFAA TIBA VYA MILIONI 74


Na WILLIUM PAUL, MOSHI.

SERIKALI imeendelea kuboresha huduma za afya katika jimbo la Vunjo wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo imetoa vifaa tiba katika kituo cha Afya cha Himo vyenye dhamani ya milioni 74 pamoja na gari la kubebea wagonjwa.

Akikabidhi vifaa hivyo, Mbunge wa Jimbo hilo, Dkt. Charles Kimea alisema kuwa, kutolewa kwa vifaa hivyo vitasaidia kituo hicho cha afya kutoa huduma bora kwa wananchi kwani kipo katikati ya Jimbo hilo ambapo wananchi wa kata nyingi hutegemea huduma hapo.

“Tunamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan hata mimi nilikuwa na wasiwasi hata nilipomuomba kukipandisha hadhi kuwa kituo cha Afya haikuwa na majengo ya Wodi , maabara jengo la mama na mtoto pamoja na mochwari lakini kwa sasa serikali imeanza kuboresha kwa kuleta vifaa tiba” alisema Dkt. Kimei.

Mbunge huyo alisema kuwa, katika kampeni za mwaka 2020 walifika kituo hapo na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwine Mollel na kumweleza shida na adha zilizokuwa zikiwakumba wananchi ambapo kitua hicho kilikuwa hakituo huduma masaa 24 na kuomba kipandishwe hadhi.

Alisem kuwa, katika jimbo la Vunjo baada ya sense ya watu 2022 ilionyesha kuwa katika jimbo hilo kulingana na idadi ya watu kila kata ilistaili kuwa na kituo cha afya ambapo tatizo lilionekana zipo kata hazina maeneo ya kujengewa vituo vya afya hivyo kwa sasa wamelenga kuboresha kati zenye maeneo kwa kujenga vituo vya afya.

Aliongeza kuwa, baada ya kupata vifaa tiba hivyo kituo hicho cha Afya ktalazimika kuongezewa wataalam wa afya ambao watatumia vifaa hivyo kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi katika kituo hicho, Dkt. Sudi Mohamed alisema kuwa, wamepokea vifaa tiba ambavyo ni drip stendi, mashuka 60, magodoro 15, vifanda vya wagonjwa na vifaa vingine ambapo alisema kuwa vifaa hivyo vitasaidia kuboresha huduma kwa wananchi .




«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: