HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

SPIKA NDUGAI AONGOZA WABUNGE KATIKA MECHI KATI YA TIMU YA BUNGE NA TIMU YA FC GRACE UNITED STATES KUTOKA NCHINI MAREKANI ILIYOFANYIKA LEO KATIKA UWANJA WA JAMHURI MJINI DODOMA.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Mchezaji wa timu ya Bunge Mheshimiwa William Ngeleja (kushoto) wakati akikagua vikosi vya timu ya Bunge pamoja na timu ya FC GRACE UNITED STATES kutoka nchini Marekani kabla ya kuanza kwa mechi yao iliyofanyika leo katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akionyesha zawadi ya jezi ya timu ya Taifa ya Marekani aliyopewa na Mchezaji wa timu ya FC GRACE UNITED STATES Ndg. Robert Allen (kushoto) kabla ya kuanza kwa mechi kati ya timu ya Bunge pamoja na timu ya FC GRACE UNITED STATES kutoka nchini Marekani iliyofanyika leo uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akikabidhiwa jezi na Mchezaji wa timu ya FC GRACE UNITED STATES Ndg. Robert Allen (kushoto) kabla ya kuanza kwa mechi kati ya timu ya Bunge pamoja na timu ya FC GRACE UNITED STATES kutoka nchini Marekani iliyofanyika leo uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia)akifurahia jambo na Mchungaji Vicent Valentyn kutoka Afrika kusini (watatu kulia) wakati wakifuatilia mechi kati ya timu ya Bunge pamoja na timu ya FC GRACE UNITED STATES kutoka nchini Marekani iliyofanyika leo uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akikabidhiwa Mipira kutoka kwa Ndg. Robert Allen (kulia) kwa ajili ya timu ya Bunge, kabla ya kuanza kwa mechi kati ya timu ya Bunge na timu ya FC GRACE UNITED STATES kutoka nchini Marekani  iliyofanyika leo uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

SPIKA WA BUNGE AONGOZA KIKAO CHA UONGOZI WA BUNGE

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi kilichokutana jana usiku katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma, kulia ni Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Kazi, Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama.
 Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge wakiwa tayari kwa ajili ya kuanza kwa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika jana usiku katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma.

SPIKA NDUGAI APATA UGENI KUTOKA BUNGE LA MSUMBIJI LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias (katikati) pale ugeni kutoka kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Beatriz Chaguala.
  Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisisitiza jambo mbele ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji uliomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, katikati ni Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias na kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Beatriz Chagula.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akizungumza  mbele ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, wa pili kushoto ni Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

SPIKA NDUGAI APATA UGENI KUTOKA TAASISI YA UTSS (UNDER THE SAME SUN) LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Peter Ash (kushoto) pale ugeni kutoka Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Peter Ash (kushoto) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Peter Ash (katikati) pale ugeni kutoka Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Vicky Ntetema 
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka Taasisi ya UTSS (Under the same Sun) ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi hiyo Ndg. Peter Ash (wa tatu kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Vicky Ntetema (wa tatu kulia) baada ya kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Spika awaonya wapinzani wanaotaka marais wastaafu washtakiwe

Spika wa Bunge, Job Ndugai amewakumbusha wabunge wa upinzani wanaotaka marais wastaafu washtakiwe kuhusu sakata la mchanga wa madini, wakumbuke wanao mawaziri wakuu wastaafu wawili ambao watahusika pia.
Ndugai amesema hayo leo (Jumanne) bungeni baada ya mchango wa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali kusema haiwezekani mawaziri na watendaji wengine wa Serikali wakafanikisha mikataba mibovu ya madini bila ridhaa ya Rais.
"Haiwezekani mzee wangu (Andrew) Chenge na (Nazir) Karamagi walipitisha mikataba hiyo bila Rais aliyekuwapo kufahamu. Kinga ya Rais kushtakiwa iondolewe ili wahojiwe," amesema Lijualikali.
Baada ya hoja hiyo ya Lijualikali inayofanana na ya Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Ndugai aliwakumbusha juu ya mawaziri wastaafu walionao kwenye chama chao.
"Mabadiliko mnayoyataka yakipitishwa na viongozi mlionao wakikamatwa msije mkalalamika tena," amesemaNdugai.

SPIKA NDUGAI ATEMBELEWA NA BALOZI MDOGO WA MAREKANI NCHINI TANZANIA LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Balozi mdogo wa Marekani nchini Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Inmi Patterson, pale alipomtembelea leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akipokea zawadi ya saa kutoka kwa Balozi mdogo wa Marekani nchini Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Inmi Patterson, pale alipomtembelea  leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo pale alipotembelewa na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini Tanzania, wakiongozwa na Balozi wa Uingereza nchini, Mheshimiwa Sarah Cooke(kulia kwake) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mheshimiwa Sarah Cooke (wa pili kushoto) pale Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini Tanzania walipomtembelea leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza na Balozi kutoka Norway, Mheshimiwa Hanne Kaarstad (katikati) na Balozi kutoka Finland Mheshimiwa, Pekka Hukka (kulia) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mheshimiwa Hawa Ghasia (wa pili kulia) akiongoza kikao cha pamoja cha mashauriano kati ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti pamoja na Wadau wa Mashirika ya Maendeleo Duniani, kutoka Benki ya Dunia (World Bank) na Shirika la fedha la kimataifa (IMF) kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti na Wadau kutoka Mashirika ya Maendeleo Duniani wakiwa katika kikao cha Mashauriano ya pamoja kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

SPIKA NDUGAI APATA UGENI WA BALOZI WA MOROCCO NCHINI TANZANIA PAMOJA NA KATIBU MKUU WA CCM TAIFA LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Mheshimiwa Abdelilah Benryane (kushoto) pale alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akizungumza jambo pale alipopata ugeni wa  Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Mheshimiwa Abdelilah Benryane (kushoto) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akimsikiliza Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Mheshimiwa Abdelilah Benryane (kushoto) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Ndg. Abdulrahman kinana (kulia) pale alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akisisitiza jambo pale alipopata ugeni wa Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Ndg. Abdulrahman kinana (kulia) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akipiga picha ya pamoja na katibu Mkuu wa CCM Taifa, Ndg. Abdulrahman kinana (kulia) pale alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, kushoto ni katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)


SPIKA NDUGAI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI NA KAMATI YA BAJETI LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akiongoza kikao cha kamati ya Uongozi na kamati ya Bajeti leo Ofisini kwake Mjini Dodoma kulia kwake ni Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa na Kushoto kwake ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah na anaefuata ni Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Bavicha wamjia juu Spika Ndugai kumtoa Mnyika bungeni

Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), limeaalani kitendo cha udhalilishaji kilichofanywa na Spika wa Bunge, Job Ndugai cha kumtoa kwa nguvu jana Waziri Kivuli wa Wizara ya Madini na Nishati, John Mnyika.
Kauli hiyo imetolewa leo Jumamosi na Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Katambi wakati akizungumza na wanahabari katika makao makuu ya chama hicho Kinondoni.
Katambi amesema Ndugai hakutumia busara kumtoa Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Kibamba, bali alikuwa na jazba katika kutoa uamuzi huo wa mbunge.
“Adhabu ya Mnyika kutoka nje ya Bunge ilitosha kabisa. Lakini si kumwambia asihudhurie vikao kwa siku kadhaa,” amesema Katambi.
Amesema ni wakati mwafaka wa Ndugai kufanya upya marejeo ya uamuzi aliyoutoa ambao kwa anadai ulikuwa wa jazba kuliko busara.
Hata hivyo, Katambi amesema vita ya madini haiwezi kufanikiwa kwa kuwatoa wapinzani nje ya Bunge ambao wana mawazo mbadala ambayo yanaweza kuwasaidia kwa namna moja au nyingine.
“Tunasikitika na kitendo kilichofanywa na Ndugai, nadhani busara alizisahau nyumbani basi angejaribu hata kuzikumbuka kuliko kutoa uamuzi kama ule."

SPIKA WA BUNGE ATEMBELEWA NA MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO LEO MJINI DODOMA.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Mchungaji Anthony Lusekelo (kulia) alipomtembelea leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akizungumza jambo wakati alipotembelewa na ugeni kutoka Kanisa la Maombezi (GRC) ulioongozwa na Mchungaji Anthony Lusekelo (wa pili kulia) katika kikao kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia) akimsikiliza Mchungaji Anthony Lusekelo (kulia) kutoka Kanisa la Maombezi (GRC) pale alipomtembelea leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kushoto)akimsikiliza Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Anna Lupembe (aliesimama)akizungumza jambo pale ugeni kutoka kanisa la Maombezi (GRC)ukiongozwa na Mchungaji, Anthony Lusekelo (wa pili kulia)ulipomtembelea leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akipiga picha ya pamoja na ugeni kutoka Kanisa la Maombezi (GRC) ukiongozwa na Mchungaji Anthony Lusekelo (wa tatu kulia) baada ya kikao kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

SPIKA WA BUNGE MH. JOB NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA RAIS WA KENYA


  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai akisalimiana na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta wakati wa ibada Maalum ya kuliombea Taifa la Kenya iliyoandaliwa na Bunge la nchi hiyo. Wengine katika  pichani kutoka kushoto ni Spika wa Bunge la Kenya  Justin Muturi, Spika wa Bunge la Seneti la Kenya Mhe  Ekwee Ethuro na Jaji Mkuu wa Kenya Jaji David Maraga. Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai (katikati ya waliokaa kulia) akizungumza na Rais wa Kenya Mhe Uhuru Kenyatta na Makamu wake Mhe William Rutto walipokutana wakati wa ibada Maalum ya kuliombea Taifa hilo. Wengine katika picha ni Spika wa Bunge la Kenya  Mhe Justin Muturi (kulia kwa Mhe Ndugai),Spika wa Bunge la Seneti la Kenya   Mhe. Ekwee Ethuro  (wa kwanza kulia),Mke wa Rais wa Kenya Margaret Kenyatta na Mke wa Makamu wa Rais wa Kenya Rachel Chebet.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (wa pili kulia) Mhe Job Ndugai akizungumza na Spika wa Bunge la Seneti la Kenya Mhe Ekwee Ethuro  (wa pili kushoto). Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai akizungumza na Spika wa Bunge la Seneti la Kenya Mhe Ekwee Ethuro  alipomtembelea Ofisini kwake Jijini Nairobi, Kenya. Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la nchi hiyo.

(Picha na Ofisi ya Bunge)

SPIKA MHE. JOB NDUGAI ATEMBELEA BUNGE LA KENYA

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai  (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kuhusu Bunge la Kenya linavyofanya kazi kutoka kwa Spika wa Bunge hilo Mhe Justin Muturi.Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job akipokea zawadi kutoka Spika wa Bunge la Kenya Mhe Justin Muturi.

(Picha na Ofisi ya Bunge)

MHE SPIKA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA BALOZI WA PALESTINA OFISINI KWAKE JIJINI DAR ES SALAAM

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akizungumza na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hazem M. Shabat, ofisini kwake jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Bunge).
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akimsikiliza  Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hazem M. Shabat,  wakati alipozungumza naye ofisini kwake jijini Dar es Salaam. 
 Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hazem M. Shabat akimueleza jambo Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai wakati akimkabidhi barua Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hazem M. Shabat akimkabidhi Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai kitabu mara baada ya kuzungumza naye Ofisini kwake jijini Dar es Salaam. 

SPIKA WA BUNGE ATEMBELEWA NA WABUNGE WA BUNGE LA UMOJA WA ULAYA

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya Mhe. Alojz Peterle (kulia) pale ugeni wa Wabunge kutoka Bunge la Umoja wa Ulaya ulipomtembelea leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo pale ugeni wa Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya ulipomtembelea leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza  jambo pale alipopata ugeni wa Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya, katika Kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wanne kulia) akipiga picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya wakiongozwa na Mhe. David Martin (wanne kushoto) baada ya kumalizika kikao kilichofanyika  leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
Wageni wa Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai ambao ni Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya wakifwatilia Vikao vya Bunge vinavyoendelea leo Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE) ​