HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 31/10/2012


.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.
.

.

JACK WOLPER: ''NIMECHOKA KUTAPELIWA KIMAPENZI NA SIHITAJI KULIA TENA"

Wapambe kadhaa wa msanii Jackline Wolper wamelonga na mwandishi wetu  kuwa, hivi sasa Wolper haitaji kulia tena kwenye mapenzi hivyo amepanga mwanaume ambaye atamtangaza muda wowote basi watu wajue kuwa ndiye mume kabisa kwani haitaji tena kuumizwa.


Wapambe hao ambao mara nyingi huwa karibu na msanii huyo, walifunguka kuwa kwa sasa msanii huyo hana mwanaume na endapo akimpata basi ataamua kufanya hivyo ili kuzuia matatizo mengine yanayoweza kutokea kama kuibiwa na watoto wenyewe njaa kali wanajifanya wamesomea mapenzi.


Hata hivyo walidai kuwa kingine ambacho msanii huyo hataki kukosea tena ni kumtangaza mpenzi wake kwa mademu wa bongo movie kwani wanahusika mara kadhaa kwa kuharibu mapenzi yake kwani hawakawii kufanya mapinduzi.


“Ishu iko hivyo mjini hapa kila mtu ana mipango lakini kwa upande wa mwanadada Wolper mambo yako hivyo na hataki kupoteza muda kwa sababu mademu wa tasnia hiyo wana tabia ya kumzoea mtu kwa dakika kadhaa baada ya hapo kwisha habari wanaondoka mwanaume kama hawana akili nzuri,”
alisema mpambe.

Hata hivyo mwandishi wa habari hizi alimtafuta
Wolper ili kutoa la moyoni naye alidai kuwa lisemwalo lipo na kama halipo basi linakuja hivyo anachopanga sasa anaamini kitatimia kwani amechoka na wezi wa mapenzi ambao mwisho wa siku wanaachana kwa vita na maneno ya kudhalauliana.
 
CHANZO: MPEKUZI

Rushwa nje nje uchaguzi wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima 

WAPAMBE NUSURA WAZICHAPE KAVUKAVU, UCHAGUZI KUFANYIKA DODOMA LEO

WAKATI uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ukifanyika leo, suala la rushwa, makundi na wajumbe kutaka kuzipiga yalitawala jana.
Uchaguzi huo wa wazazi ndiyo wa funga dimba la mfululizo wa chaguzi za chama hicho tawala kuanzia ngazi za shina tangu Aprili.
Tuhuma hizo za rushwa zimejitokeza licha ya juzi wagombea mbalimbali kukaririwa wakiyakana makundi ambayo yamekuwa yakitajwa kuwa na ajenda maalumu ya kusaka urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kupitia chama hicho.
 
Kampeni na rushwa
Mmoja wa wajumbe kutoka mkoani Iringa alimwambia mwandishi wetu kuwa tayari baadhi ya wajumbe wanaoonekana kuwa na msimamo mkali wamekuwa wakipewa Sh100,000 kila mmoja wakati wajumbe wengine wamekuwa wakihongwa kati ya Sh40,000 na 70,000.
“Nikimwona Rais Jakaya Kikwete nitamwambia. Hali hii siyo nzuri na haiwezi kuvumiliwa. Kama alivyosema juzijuzi hapa nilimsikia, lazima achukue hatua, la sivyo chama chetu kitakufa,” alisema mjumbe huyo ambaye aliomba asitajwe jina.
Katika hatua nyingine, makundi ya baadhi ya wajumbe waliokuwa wameketi katika moja ya baa maarufu mjini Dodoma, juzi usiku walitimka mbio baada ya kuona gari likiegeshwa pembezoni mwa baa hiyo.
Wajumbe hao waliokuwa kwenye harakati za kupanga mikakati ya kuzunguka katika nyumba za kulala wageni kwa ajili ya ‘kuonana’ na wajumbe, walitimka wakidhani kuwa gari hilo lilikuwa na maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Wagombea wanaowania uenyekiti, John Barongo na Abdallah Bulembo juzi, kwa nyakati tofauti walikanusha kuwa na maslahi na makundi yanayodaiwa kushiriki katika vitendo vya kutoa rushwa katika uchaguzi huo unaofanyika leo. Mgombea mwingine wa nafasi hiyo, Martha Mlata alikataa kuzungumzia uchaguzi huo.
Uchaguzi huo, unahitimisha uchaguzi wa jumuiya tatu za chama hicho, baada ya ule wa UWT na UVCCM ambazo zilizua malalamiko kutokana na kutawaliwa na madai ya rushwa.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akifunga mkutano wa UWT na baadaye alipofungua ule wa UVCCM,   alikemea vitendo hivyo na kueleza athari za rushwa katika chaguzi za chama.

Mchuano wa Wabunge

Kama ilivyokuwa katika uchaguzi wa UWT, mchuano mwingine mkali unaonekana katika kinyang’anyiro cha ujumbe wa Nec, huku kukiwa na idadi kubwa ya wabunge wanaowania nafasi hiyo.
Majina 16 yamepitishwa kuwania viti vitatu vya Nec kwa upande wa Tanzania Bara, wakati kwa upande wa Tanzania Visiwani majina yaliyopitishwa ni saba kugombea nafasi mbili.
Miongoni mwa wanaowania nafasi tatu Bara ni Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu, Stella Manyanya na Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu.
Pia wamo wabunge ambao majimbo yao yapo kwenye mabano Said Bwanamdogo (Chalinze), Vita Kawawa (Namtumbo), Murtaza Mangungu (Kilwa Kaskazini) na Mbunge wa zamani wa Viti Maalumu, Esther Nyawazwa.
Wengine katika kundi hilo ni Norad Kigola, Priscilla Mbwaga, Dk Salim Chikago, Jeremia Wambura, Bernard Murunya, Thobias Mwilapwa, Paulo Kirigini na Clementina Mollel.
Kutoka Zanzibar, wanaowania nafasi mbili za Nec ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Perera Ame Silima, Abdulla Khamis Feruz, Ali Suleiman Othman, Fatuma Abeid Haji, Panya Ali Abdalla, Twaha Ally Muhajir na Hassan Rajab Khatib.
Pia mkutano wa leo unatarajiwa kumchagua Makamu Mwenyekiti, nafasi inayowaniwa na Hassan Rajab Khatib, Ali Issa Ali na Dogo Iddi Mabrouk.
Utawachagua pia wajumbe wa Baraza Kuu la Wazazi na wawakilishi wa jumuiya hiyo katika mabaraza ya UVCCM na UWT.

Vijembe vya Kampeni
Kampeni zimekuwa zikipamba moto kadri muda wa uchaguzi unavyokaribia na mbinu mbalimbali zimekuwa zikitumika ili kujihakikishia ushindi.
Magari mengi yamepambwa picha nyingi za wagombea, wapambe wanapita sehemu mbalimbali kuomba kura na kuta za uzio wa ofisi za CCM zimechafuka kwa picha za wagombea.
Ushindani mkubwa unaonekana kuwa baina ya Barongo na Bulembo ambao jana walikuwa kivutio kikubwa walipokutana katika ofisi za CCM Makao Makuu, Dodoma ambako walikumbatiana kisha kuanza kurushiana vijembe.
Bulembo alisema: “Nilipomkuta anachukua fomu, nilimwuliza mwalimu wangu huyu (Barongo) kwamba nilidhani kwamba sasa unaniachia nikutue mzigo, kumbe bado tena nawewe unagombea?”
Barongo alimjibu akisema: “Hilo haliwezekani kabisa, ujue ninyi bado watoto hamjakomaa bado mnahitaji kuongozwa, kwa hiyo wewe tulia kwanza muda mwafaka ukifika nitakukabidhi.”
Jana asubuhi, Bulembo alifika katika Viwanja vya Bunge kuomba kura kwa baadhi ya wabunge ambao ni wajumbe wa mkutano mkuu wa jumuiya hiyo.
Muda mfupi kabla ya wabunge kuingia ukumbini, Bulembo alikuwa nje ya lango kuu la kuingilia kwenye ukumbi wa Bunge na kila mbunge aliyejitokeza alimsalimia kisha kuomba kura kwa wale ambao ni wajumbe hao.
Mlata jana kwa muda mrefu hakuonekana katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM na taarifa zinasema huenda alikuwa akihudhuria kikao cha Baraza Kuu la Jumuiya hiyo kilichofanyika jana katika Chuo cha Mipango.
Licha ya kutokuwapo kwake, kulikuwa na vijana wachache waliokuwa wamevalia mabango makubwa yenye picha yake, vifuani na kwenye migongo yao wakimpigia kampeni.
Wafuasi nusura wazichape
Wakati Bulembo na Barongo wakirushiana vijembe kwa furaha, watu wanaoaminika kuwa ni wafuasi wao nusura wachapane makonde walipokuwa wakiimba nyimbo za hamasa CCM Makao Makuu.
Wafuasi hao jana walikuwa wakizunguka wakiwa na mabango yenye kuwanadi wagombea hao katika ofisi hizo kati ya saa sita na saa nane mchana huku wakiimba nyimbo za hamasa.
Hali hiyo ilisababisha kutosikilizana katika eneo hilo, hivyo kuwalazimu maofisa wa CCM kuviamuru kuondoka na kuelekea katika mbele ya jengo la vikao vya NEC maarufu kama White House. Viliitikia wito na kwenda huko ambako viliendelea kuimba nyimbo za hamasa.
Wakati vikiwa katika eneo hilo, wafuasi hao walianza kurushiana maneno makali kwa huku kila upande ukidai kufanyiwa rafu na upande mwingine, hali iliyozua tafrani iliyodumu kwa zaidi ya dakika 20.
Hata hivyo baadhi ya makada wa pande hizo mbili, walitumia busara na kuwatuliza na kila kikundi kuelekea upande tofauti na kuhitimisha shamrashara hizo.
 
CHANZO: MWANANCHI

RATIBA YA MKUTANO WA TISA WA BUNGE TAREHE 30/10/2012 MPAKA 09/11/2012

 

TAARIFA KWA UMMA


Mchungaji Lwakatare Atoa Ujumbe Wa Amani


Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni Mh. Dkt. Getrude Rwakatare akitoa Ujumbe kwa Watanzania waliohudhiria Ibada Maalum ya Kuliombea Taifa ambapo ametaka watu kutobaguana kwa misingi ya Dini, Ukabila wala Siasa na kusema pamoja na Utawala bora pia tunahitaji maombezi ili tuweze kufikia Malengo yaliyokusudiwa kulipeleka Taifa linapotakiwa kufikia.
Dkt. Rwakatare amesema nia kubwa ya kufanya Ibada hiyo ya Maombezi ni kutaka kuweka usawa kutokana na siku za hivi karibuni kuibuka kwa Matamko mbalimbali kutoka kwa watu tofauti wakiwemo viongozi wa Kitaifa, Kidini na wa baadhi ya Makundi yanayohitilafiana na kusema tukiomba kwa jina la Mungu kila kitu kitakwenda kama tulivyomuomba ili Tanzania iendelee kuwa nchi ya Amani na Utulivu kama ilivyokuwa miaka yote ambayo ni kimbilio la watu wa Mataifa mbalimbali kwa sababu Watanzania hawajui kuchukiana na wamekuwa watu wa kushikamana kwa miaka yote

Kova kuanza kusaka mtandao wa vipeperushi

Kamanda Kova 


POLISI nchini wamepanga kusambaratisha mtandao unaodhamini na kuchapisha vipeperushi vinavyohamasisha kufanyika kwa maandamano, kutaka kutolewa kwa Katibu wa Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda  Issa Ponda na wenzake.
Hatua hiyo imekuja baada ya waumini hao kupanga kufanya maandamano  Novemba Mosi, ambayo yatahamasisha mahakama hiyo kutoa dhamana kwa kiongozi wa taasisi hiyo na wenzake.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Suleiman Kova alisema wataanza kufanya msako wa wote wanaohamasisha, wanaochapisha na wanaotoa vipeperushi ili kuwakamata.
“Tunafuatilia wadhamini na wachapishaji wa vipeperushi kwani ni chanzo cha uchochezi na upotevu wa amani nchini,” alisema Kova.
Kova alisema maandamano hayo ambayo yamepangwa na waumini hao yanatishia amani , wananchi watashindwa kwenda kazini na kurudisha nyuma maendeleo ya nchi.
“Hatuna mazungumzo tena kwa suala lolote litakalotishia uvunjifu wa amani hasa kwa yeyote atakayefanya maandamano bila kibali, hatutangalia anatoka dini gani au chama gani hivyo polisi itafanya kazi yake na kuwachukulia hatua kali,” alisema Kova na kuongeza:
“Kisheria kumtishia mtu siyo lazima utumie bomu, bali unaweza ukatumia kauli au vipeperushi kama hivyo vya maandamano.”
Alisema wazazi watakaoruhusu watoto wa shule kufanya maandamano watachukuliwa hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani, ikiwezekana  kufungwa mwaka mmoja jela.
“Nimesikia wanataka kuwahusisha watoto wasiende shule, ili wafanye maandamano ambayo yanazuiwa na sheria ya mtoto kutofanya maandamano,” alisema Kova na kuongeza:
“Sisi tutahakikisha sheria inachukua mkondo wake, kama kuna mtu amefikishwa mahakamani kuna taratibu zake za kupata dhamana, siyo kufanya maandamano haramu.”
Pia, aliwaomba wananchi wasishiriki maandamano hayo kwani yataleta madhara makubwa kwa familia zao kwa wale watakaokamatwa.
“Hii inajidhihirisha pale utakapotembelea familia za wale waliokamatwa katika maandamano yaliyopita, watoto wanashindwa hata kwenda shule kutokana na kukamatwa kwa wazazi wao na wanakosa nauli na chakula,” alisema Kamanda Kova.
Pamela Chilongola, Nuzulack Dausen na Zaina Malongo

INJINIA MANYANYA AJITOSA KUTETEA NAFASI YAKE YA UJUMBE WA NEC TAIFA KUPITIA JUMUIYA YA WAZAZI

Injinia Stella Martin Manyanya ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, MNEC Jumuiya ya Wazazi toka mwaka 2007, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, Mjumbe wa SADC PF na Msimamizi wa Kimataifa wa Uchaguzi kupitia vionjo vya Uhandisi, Ujasiriamali na Sanaa alivyokuwa navyo ameamua kujitosa tena kwenye uchaguzi wa kutetea nafasi yake ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia Jumuiya ya Wazazi katika uchaguzi utakaofanyika kesho tarehe 31/10/2012 Mkoani Dodoma. 
 
Vionjo vyake katika sanaa
 
Wasifu wake
 
Anaomba kura yako

Kuna Uhaba Mkubwa Wa Mafuta Nchini Kwa Sasa

 
Kwa siku nne sasa Iringa imekuwa na uhaba wa disel na petrol. Tatizo linaripotiwa kuwemo katika sehemu nyingine za nchi.  Jana nilishindwa kabisa kupata mafuta Iringa. Nilikuwa na mafuta ya kuweza kunifikisha Ilula tu. Hapo nilidhani kungekuwa na kit uo chenye mafuta. 

Hapana! Bahati nzuri dereva wa basi la kwenda Uhambingeto aliweza kunisaidia kwa kuniuzia lita zake ishirini za dizeli. Zinifikisha Mikumi. Pale Mikumi nikafanikiwa kupata mafuta ya kununua kituoni. Vinginevyo, kwa mara ya kwanza jana nimelazimika kununua mafuta ya ' kulanguliwa'. Lita moja kwa shilingi elfu tatu. Hakyamungu! 

  Songea

Mjini Singida

Askari polisi wa mjini Singida akisimamia ugawaji wa petrol jana (29/10/2012)  kwenye kituo cha mafuta cha Esso.
Baadhi ya wafanyabiashara wa bodaboda mjini Singida,wakiwa kwenye foleni jana (29/10/2012) wakisubiri kuuziwa petrol.Kwa zaidi ya wiki tatu,kumekuwa na uhaba mkubwa wa nishati ya mafuta kitendo ambacho kimeathiri shughuli nyingi za kiuchumi kwa wakazi wa mji wa Singida na vitongoji vyake.

Wingu laigubika Ripoti ya Ngwilizi


                                                Spika wa Bunge, Anne Makinda 


WAKATI Bunge likianza mkutano wake wa Tisa leo, zipo taarifa Ripoti ya Kamati  ndogo iliyoundwa kuchunguza tuhuma za wabunge kujihusisha na vitendo vya rushwa haitasomwa na kisha kujadiliwa.
Badala yake, kwa mujibu wa watoa habari wetu, Kamati ya Uongozi, iliyokutana jana iliamua kwamba litatolewa tamko kuhusu ripoti ya kamati hiyo, hivyo haitasomwa wala kujadiliwa kama ambavyo wabunge wamekuwa wakitaka.
Kwa maana hiyo Spika wa Bunge, Anne Makinda huenda akatumia kanuni nyingine kutoa tamko kuhusu uchunguzi huo, hali ambayo haitatoa fursa kwa wabunge kuijadili kama ambavyo baadhi yao wamekuwa wakishinikiza.
Miongoni mwa kanuni ambazo Spika anaweza kuzitumia ni pamoja na ile ya 33 (2) ambayo inasema: “Wakati wa kikao, Spika anaweza kutoa taarifa nyinginezo kadri atakavyoona inafaa.”
Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel jana alikataa kuzungumzia suala hilo akiahidi kulitoa ufafanuzi leo... “Ratiba ya shughuli za Bunge bado iko kwenye ngazi ya Kamati ya Uongozi. Sasa pengine tusubiri kesho (leo) ikiwa tayari kila kitu kitakuwa wazi, hakuna haja ya kuwa na haraka.”
Jana, Kamati ya Uongozi wa Bunge ilikutana mjini Dodoma kujadili mambo mbalimbali na habari zinasema kwamba suala la Ripoti hiyo ya Ngwilizi, pia lilijadiliwa.
Agosti 2 mwaka huu, Spika Makinda aliunda kamati hiyo ndogo kuchunguza tuhuma za rushwa zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya wabunge ambao walidaiwa kwamba walihongwa ili kuikwamisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.
Kuundwa kwa kamati hiyo, kulitanguliwa na tukio la kuvunjwa kwa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Julai 28, mwaka huu pia kutokana na tuhuma hizohizo.
Tayari kumekuwa na taarifa kwamba ripoti hiyo imevuja na maudhui yake kuchapishwa katika baadhi ya vyombo vya habari, hali ambayo ilisababisha Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kuonya kwamba waliohusika na kuvuja huko huenda wakajikuta matatani kwani ni kosa la kisheria.
“Kitendo cha kuchambua na kuchapisha maudhui ya taarifa hiyo katika vyombo vya habari ni kinyume cha sheria na kinaingilia uhuru, haki na madaraka ya Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 31 (1) (g) cha Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge Sura 296,” alisema Ndugai katika mkutano wake na waandishi wa habari hivi karibuni.
Mmoja wa wabunge ndani ya kamati iliyochunguza suala hilo (jina tunalihifadhi kwa sasa), ndiye anayedaiwa kwamba aliivujisha ripoti hiyo ya uchunguzi kwa makusudi, lengo likiwa ni kumshinikiza Spika Makinda aitoe hadharani ili kuwasafisha watuhumiwa.
Mbunge huyo alifanya hivyo kwa msukumo wa baadhi ya wabunge waliotuhumiwa kujihusisha na rushwa, pamoja na baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kabla ya kuvunjwa.
Kadhalika, Ndugai katika mkutano wake na vyombo vya habari alisema suala la ripoti hiyo kusomwa bungeni au vinginevyo linategemea uamuzi wa Kamati ya Uongozi ya Bunge.
Ndugai alisema baada ya kamati kuwasilisha ripoti kwa Spika, Kamati ya Uongozi ya Bunge itakaa kujadili na kama itaona kuna umuhimu wa kuingizwa katika ratiba ya vikao vya Bunge ijadiliwe.
Alisema Vifungu 114 (17) na 119 (1) hadi (6) vya Kanuni za Bunge, Toleo la 2007 kwa pamoja vinampa madaraka Spika kuhusu utaratibu wa kufuata katika uwasilishaji wa taarifa bungeni.
Kamati hiyo iliyoundwa na Spika ilikuwa chini ya Ngwilizi ambaye ni Mbunge wa Mlalo, ina wajumbe; Said Arfi (Mpanda Kati), John Chiligati (Manyoni Mashariki), Goesbert Blandes (Karagwe) na Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Omary Juma. Kamati hiyo ilimaliza kazi yake na kuiwasilisha kwa spika tangu Septemba 20 mwaka huu.

Kamati za Vyama


Kamati za vyama bungeni zinatarajiwa kufanya vikao vyake leo asubuhi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Ofisa Habari wa Bunge, Prosper Minja alisema
Kamati nyingine za Bunge hazijakutana kutokana na wabunge wengi kuwa safarini kwenda mjini Dodoma kuhudhuria kikao cha Bunge.
“Kwa taarifa tulizopokea sasa ni kwamba kamati zimeshindwa kukutana kutokana na wabunge wengi kuwa njiani kuja mjini hapa, hivyo kwa vyovyote kesho (leo) Bunge litakuwa ni fupi ili wabunge wapate nafasi ya kuandaa utaratibu mzima wa ratiba za vikao,” alisema Minja.
Alisema leo mara baada ya kuanza kwa kikao hicho, Bunge litatoa nafasi ya maswali na majibu ambayo Serikali itayajibu kabla ya kuahirishwa.
Mara baada ya kuahirishwa saa nne asubuhi, kamati za vyama zitakutana kupitia mambo mbalimbali kabla ya kuingizwa kwenye kamati mbalimbali za bunge.
Moja ya mambo yanayotarajiwa kutawala katika kamati za vyama ni pamoja na wabunge wa CCM kujiweka sawa kwa ajili ya kusaidia kupitishwa kwa ripoti ya Kamati ya Ngwilizi.
Kingine kitakachojadiliwa katika Mkutano huu wa Bunge ni muswada binafsi kuhusu fao la kujitoa la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Tayari Mbunge wa Kisarawe, Suleiman Jaffo na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika wamewasilisha miswada yao kwa Katibu wa Bunge, Tomas Kashillilah.


CHANZO: MWANANCHI

Mjomba Kumbuka Japo Wanao.....

Mfanyakazi wa Barrick mwaathirika wa kemikali afariki

 Samuel alifariki Oktoba 25  saa 2:00 usiku. 
MFANYAKAZI wa Kampuni ya Africa Barrick Gold aliyekuwa akifanya kazi mgodi ya Bulyanhulu, wilayani Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Samuel Kamudulu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu akisumbuliwa na mapafu na uti wa mgongo.
Akizungumza kwa simu kutoka Arusha, kaka wa marehemu, Lekiu Kamdulu  alisema Samuel alifariki ghafla walipokuwa Arusha baada ya kutoka matibabu Dar es Salaam.
“Samuel alifariki Oktoba 25  saa 2:00 usiku. Unajua baada ya kumwandikia ile habari kwenye gazeti la Mwananchi, kampuni ilimchukua na kuanza kumtibu. Kwa hiyo tuliitwa Kahama tukafanyiwa utaratibu na kurudishwa tena Dar es Salaam kwenye matibabu,” alisema Kamudulu na kuongeza:
“Baada ya kutoka kwenye matibabu tulikuja Arusha nyumbani tangu wiki iliyopita hadi alipofariki juzi.”  
Wakati wa uhai wake, Samuel alisema mapafu yake yameathiriwa na kemikali zinazotumika kwenye uchimbaji madini ya dhahabu.
“Mapema mwaka huu nikiwa kazini ndani ya mgodi niliishiwa nguvu ghafla na kuanguka. Nilibebwa bila kujitambua na kupelekwa hospitali ya kazini na kuambiwa kuwa nina ugonjwa wa mapafu (pneumonia),” alisema Samuel wakati wa uhai wake na kuongeza:
“Baada ya hali kuzidi kuwa mbaya nililetwa Hospitali ya Aga Khan ambako nimeambiwa mapafu yangu yameoza kutokana na kemikali zinazotumika mgodini.”
Alipoulizwa kuhusu kifo hicho, Ofisa Habari wa Barrick, Nector Foya alisema hana taarifa za kifo cha mfanyakazi huyo.

Dodoma kuwaka moto, Bunge kuanza Mkutano wa Tisa Kesho

MKUTANO wa Tisa wa Bunge la Muungano unatarajia kuanza kesho Mjini Dodoma, huku ripoti ya Kamati Ndogo ya Bunge iliyoundwa kuchunguza tuhuma za rushwa kwa baadhi ya wabunge ikisubiriwa kwa hamu kubwa.
Tume hiyo inayoongozwa na Hassan Ngwilizi iliundwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda kwa ajili ya kuchunguza tuhuma hizo zilizoibuka katika mkutano wa Bunge uliopita. Tuhuma hizo ndizo zilizomfanya Spika kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.
Baada ya kuibuka kwa tuhuma hizo, Agosti mwaka huu, Makinda aliunda tume ya wabunge watano kuchunguza tuhuma hizo.
Ripoti hiyo inatarajiwa kuwa mtihani mkubwa kwa Spika Makinda hasa ikizingatiwa kwamba ndiye mwenye mamlaka ya kuwasilisha ripoti hiyo bungeni hasa kutokana na kuibuka kwa maneno ya chinichini kwamba kumekuwa na jitihada za kuwasafisha wabunge hasa wa chama tawala.
Hivi karibuni, Naibu Spika, Job Ndugai alikaririwa akisema kuwa mamlaka ya namna ya kuiwasilisha ripoti hiyo yako mikononi mwa Spika Makinda.
“Kwa kawaida na kanuni zetu ni kwamba Spika anaweza kuamua kama ripoti hiyo ijadiliwe au iwasilishwe kwa njia ipi, wala hawezi kuingiliwa,” alisema Ndugai.
Mbali na ripoti hiyo, Mkutano huo wa Bunge ambao utadumu kwa wiki mbili, pia unatarajiwa kupokea hoja binafsi kutoka kwa Mbunge wa Kisarawe (CCM), Suleiman Jaffo kuhusu mifuko ya jamii.
Jaffo aliibua hoja hiyo katika mkutano uliopita akitaka itungwe sheria ya kufanya marekebisho ili kipengele kinachomtaka mwanachama wa mfuko kupewa mafao yake pindi anapofikisha umri wa miaka 55 kiondolewe.
Wakati huohuo, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi walianza kuwasili Dodoma jana tayari kwa mkutano wa uchaguzi unaotarajia kuanza kesho.
Awali, mkutano huo uliokuwa ufanyike Oktoba 27 hadi 28, lakini ulisogezwa mbele ili kupisha waumini wa dini ya Kiislamu kuungana na wenzao duniani kusherehekea Sikukuu ya Idd El Haj.
Katika uchaguzi huo nafasi ya mwenyekiti inagombewa na Abdallah Bulembo na John Barongo na Martha Mlata.
Tayari Jumuiya nyingine za CCM za Umoja wa Vijana (UVCCM) na UWT zimeshafanya uchaguzi wa viongozi wake wa juu wa kuziongoza kwa kipindi cha miaka mitano.Katika chaguzi hizo, UVCCM ilimchagua Khamis Sadifa Juma kuwa mwenyekiti wake mpya wakati Sofia Simba alichaguliwa tena kuongoza UWT.

Vigogo 10 wahusishwa mabilioni ya Uswisi

Mheshimiwa Zitto Kabwe 

ZITTO ASISITIZA NYARAKA ZIPO, DK HOSEAH NDIYE ANAYEZIZUIA

ZA VIGOGO 10 

Vigogo wametajwa kuhusika katika kashfa ya kuficha Sh303.7 bilioni katika benki mbalimbali nchini Uswisi.
Katika orodha hiyo inadaiwa kuwa yupo kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu, maofisa watatu wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), mawaziri wastaafu ambao baadhi yao bado ni wabunge na aliyewahi kuwa kiongozi mwandamizi wa Benki Kuu Tanzania (BoT).
Majina hayo ambayo mwandishi wetu amefanikiwa kuyaona, yamo katika orodha ya mchunguzi mmoja wa kimataifa wa masuala ya ufisadi (jina tunalo).
Juzi, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alimshukia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah akimtuhumu kuandika barua Uswisi akisema Tanzania haina masilahi na mabilioni ya fedha yaliyofichwa katika benki zilizopo nchini humo. Hata hivyo, Dk Hoseah alikanusha madai hayo akisema hajawahi kufanya hivyo.
Akizungumza jana Zitto alisisitiza kauli yake akisema: “Sijawahi kumsema Dk Hoseah kwa lolote, kwa nini leo nimsingizie? Yeye mwenyewe anajua ushirikiano niliompa wakati wabunge wanapinga yeye asichunguze malipo ya posho mara mbili kwa wabunge.”
“Nilisimama kidete kusema Takukuru wapo sahihi na mimi nilikwenda mwenyewe kwao kuhojiwa na kuagiza wajumbe wa kamati yangu (Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma), waende kuhojiwa. Spika aliyestaafu (Samuel Sitta) akaizima kashfa ya wabunge kupokea posho mara mbilimbili. Mwulizeni amesahau? Sasa leo nimzushie ili iwe nini?.”
Alisema orodha ya Watanzania wenye fedha huko Uswisi, ipo na ameiona na nyaraka zinaweza kutolewa kwa taasisi za Serikali tu.
“Dk Hoseah kazuia nyaraka hizo. Akitaka nimwonyeshe mtu anayeweza kutoa nyaraka hizo, nipo tayari isipokuwa aahidi kuiweka wazi,” alisema Zitto.
Alisema katika orodha ambayo Waziri wa Fedha wa Ufaransa anayo, kuna Watanzania lakini akaituhumu Serikali akisema haitaki kufuata njia halali za kupata orodha hiyo kwa kuwa viongozi wengi na wafanyabiashara wakubwa wana akaunti katika benki za Uswisi.
Juni 26, mwaka huu gazeti hili lilichapisha habari kuhusu utoroshwaji wa fedha hizo na kueleza kuwa Polisi wa Kimataifa (Interpol) nchini kwa kushirikiana na Takukuru inachunguza suala hilo.
Kiasi hicho cha fedha kimedaiwa kuingizwa katika akaunti za Watanzania na kampuni moja ya uchimbaji mafuta na kampuni kadhaa za uchimbaji madini ambazo zinafanya kazi Tanzania.
Chanzo hicho kiliongeza kwamba kiasi hicho cha fedha kipo katika akaunti sita tofauti zinazomilikiwa na Watanzania wakiwamo wanasiasa wakubwa.
Hata hivyo, chanzo hicho kilieleza kuwa tangu akaunti hizo zifunguliwe, wamiliki wake halali hawajawahi kuingiza hata shilingi.
“Uchunguzi wetu unaonyesha kuwa fedha hizo zipo katika akaunti sita tofauti ambazo zinamilikiwa na wanasiasa wakubwa nchini na wenzetu wa Uswisi wameeleza fedha hizo zimeingizwa na kampuni kadhaa ambazo zinahusika na mafuta pamoja na madini hapa nchini,” kilidokeza  chanzo hicho.
Kugundulika kwa kiasi hicho cha fedha katika benki za Uswisi ni kutokana na ripoti ya Benki ya Taifa ya Uswisi (SNB) iliyotolewa mwaka huu.


CHANZO: MWANANCHI

Magazet Leo Jumatatu Tarehe 29/10/2012






Kichanga afariki dunia baada ya kukeketwa

“Hadi sasa tunamshikilia mama yake na watu wengine wote wakazi wa Kijiji cha Mwanyonye. Ngariba alifanikiwa kutoroka lakini tumeanzisha msako mkali kumkamata ili tuwafikishe kwenye mahakamani,” alisema.
 
WATU wawili mkoani Singida wamefariki dunia katika matukio tofauti, likiwamo la mtoto mwenye umri wa miezi minne kupoteza maisha baada ya kukeketwa.
Akizungumza ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Linus Sizumwa alimtaja mtoto aliyefariki dunia baada ya kukeketwa kuwa, ni Shamila Saidi.
Alisema tukio hilo la kinyama lilitokea Oktoba 27, mwaka huu saa 10:00 alfajiri Kijiji cha Mwanyonyi, Tarafa ya Ilongero, mkoani Singida.
Alisema siku ya tukio, mama mzazi wa mtoto huyo alimpeleka mtoto wake kukeketwa kwa ngaraiba, ili aweze kupona ugonjwa wa kuharisha na kutapika. Magonjwa hayo yanadhaniwa kusababishwa na ugonjwa wa lawalawa.
Sizumwa alisema baada ya kukeketwa, mtoto huyo alivuja damu nyingi na kusababisha kifo chake.
“Hadi sasa tunamshikilia mama yake na watu wengine wote wakazi wa Kijiji cha Mwanyonye. Ngariba alifanikiwa kutoroka lakini tumeanzisha msako mkali kumkamata ili tuwafikishe kwenye mahakamani,” alisema.
Katika hatua nyingine, Sizumwa alisema Samwel Majilala mkazi wa Kijiji cha Kideka, Kata ya Puma, Wilaya ya Ikungi ameuawa na vijana wenye hasira kwa kinachodaiwa ni kumpiga baba yake mdogo.
Alisema mauaji hayo yamechangiwa na ugomvi wa kugombea Sh600,000 ambazo babu yake alilipwa fidia ya kupisha ujenzi wa umeme wa upepo.
“Katika fidia hiyo, mtoto alipata mgawo wa Sh200,000. Mjukuu wa mzee naye alianza kuomba kupewa mgawo. Samwel baada ya kushindwa kupata mgawo huo alianza kumpiga baba yake kwa madai kuwa ni kikwazo cha yeye kukosa,” alisema.
Alisema Samwel baada ya kumpiga baba yake mdogo, alitoroka na kukimbilia Kijiji cha Dung’unyi ambako alifuatwa na kundi la vijana na alipokamatwa, alipigwa hadi kusababisha kifo chake.
Kamanda Sizumwa alisema hadi sasa wanawashikilia watu saba kuhusiana na mauaji hayo na msako zaidi unaendelea.

CHANZO: MWANANCHI

MLEZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa Mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya, Thomas Nyimbo, Ametangaza Kujivua Uanachama


MLEZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya, Thomas Nyimbo, ametangaza kujivua uanachama wa chama hicho kwa madai ya kuchoshwa na siasa za ‘Umangimeza’ ndani ya vyama vya siasa hapa nchini.


-Awaasa vijana kuwa mabadiliko ndani ya Tanzania si kuiondoa CCM na kuiweka Chadema.

Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa mbeya na iringa wakimsikiliza mlezi Thomasi Nyimbo katika ukumbi wa hotel yake ya Maunt livingstone jijini mbeya 

Raymond wa Ebony FM Iringa na Joseph Mwaisango wa Mbeya yetu wakiwa makini kumsikiliza mzee Nyimbo




MLEZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya, Thomas Nyimbo, ametangaza kujivua uanachama wa chama hicho kwa madai ya kuchoshwa na siasa za ‘Umangimeza’ ndani ya vyama vya siasa hapa nchini.

Nyimbo ambaye amewahi kuwa mbunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka 10 katika Jimbo la Njombe Magharibi kabla ya kukimbilia Chadema mwaka 2010, amesema hivi sasa atabaki kuwa mwanasiasa huru asiyefungamana na vyama.

Akitoa taarifa ya kuachana na siasa ndani ya vyama jana, Jijini hapa, huku akiwa ameambatana na mkewe Mary Mwenga, alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona siasa za kushabikia vyama hazina tija kwa watanzania walio wengi na badala yake zinawanufaisha viongozi wachahe wanaojineemesha wao wenyewe kwa kutumia jasho la wananchi.

Akifafanua zaidi alisema alichojiuzulu ni siasa za vyama, lakini sio siasa, huku akitamba kuwa yeye alizaliwa akiwa ni mwanasiasa, kiongozi na mtu ambaye mawazo yake yanahitajika kwa ajili ya maendeleo ya nchi yake, hivyo atabaki kuwa mwanasiasa asiyekuwa na chama cha siasa.

Katika taarifa hiyo aliyoitoa kwa vyombo vya habari mithiri ya Mhadhara, Nyimbo alitumia zaidi ya saa moja na nusu kuelezea mustakabali wa taifa na vijana kutokana na vyama vya siasa kuelekea kuwatumbukiza kwenye machafuko.

“Nimeachana na Chadema baada ya kubaini kuwa siasa za vyama havina tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla na ni wakati huu sasa wa kuachana na dhana ya vyama vya siasa vituandalie sera na tunahitaji sasa itungwe sera ya kitaifa ambayo mgombe inabidi atueleze tukimchagua ataitekeleza vipi” alisema Nyimbo.

Alisema hata nchi zenye wigo mpana wa Demokrasia kama Marekani ambao hivi sasa wapo kwenye mchakato wa uchaguzi Mkuu huwezi kuwasikia wagombea wake wakisifia vyama vyao, bali wanawaeleza wananchi wa Marekani watatekeleza vipi sera ya nchi yao .

Alisema kuwa ikiwa katiba mpya inayoandaliwa hivi sasa itakuruhusu mgombea huru, atakuwa tayari kugombea ubunge tena kwenye jimbo lake la Njombe Magharibi, lakini kama katiba hiyo itazuia fursa hiyo hatogomea tena wadhifa huo maisha yake yote.

Aliongeza kuwa baada ya kupatikana kwa katiba mpya, inabidi itungwe sera ya Taifa itakayolindwa kisheria, ambayo kila chama kitakachofanikiwa kuingia madarakani kilazimike kuifuata badala ya ilivyo sasa vyama vinaogelea hovyo.

Alisema kuwa ndoto za kuwa mwanasiasa huru alikuwa nazo tangu zamani, na ndiyo sababu katika mabango yake ya kuhamasisha achaguliwe wakati akigombea ubunge kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, alikuwa na kauli mbiu ya ‘Mtu kwanza, chama baadaye.
Alisema kuwa ikiwa katiba mpya inayoandaliwa hivi sasa itakuruhusu mgombea huru, atakuwa tayari kugombea ubunge tena kwenye jimbo lake la Njombe Magharibi, lakini kama katiba hiyo itazuia fursa hiyo hatogomea tena wadhifa huo maisha yake yote.

“Nitapenda kushauriana na watanzania wanaopenda maendeleo ya taifa letu nje ya mlolongo wa vyama, hivyo hata kama naipenda vipi Chadema, nalazimika kuresighn (kujiuzulu) uanachama ili niweze kutimiza azma hiyo,” alisema Nyimbo.
 
Kilicho mkimbiza Chadema.
 
Alisema ameamua kujiondoa ndani ya chama hicho baada ya kubaini kuwa kinaenda kinyume na malengo yake kama kinavyojipambanua mbele za watu.

Alisema licha ya kuwaaminisha wananchi, hususani vijana kuwa ndio chama chenye kuleta mabadiliko ya kweli,lakini viongozi wake wa daraja la juu akiwataja Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dk. Wilbroad Slaa wamekuwa wakijinufaisha binafsi.

Alisema viongozi hao pia wamekuwa si watu wa kushaurika ndani ya chama hicho, lakini kibaya zaidi ni kuendesha siasa katika mfumo mbaya wa kushawishi na kuaminisha bila kuwa na suluhisho (Mob Politics).

Alisema siasa za namna hiyo ni hatari kwa taifa kwa kuwa baada ya kuungwa mkono kwa kiwango cha juu na kundi la vijana kwa imani ya kukombolewa pale watakapofanikiwa kuingia madarakani na kushindwa kuwatimizia kutazua vurugu.

Kuhusu CCM.
 
Nyimbo alidai kuwa chama hicho kinajimaliza chenyewe kutokana na kuacha suala la rushwa kwenye chaguzi zake za ndani kuwa ndio kigezo muhimu cha kuwapata viongozi wake.

Hata hivyo alisema ili tatizo hilo limalizike ni wananchi wenyewe kuamua kuikataa rushwa kwa kupokea rushwa isiyoleta matunda kwani wakifanya hivyo watakuwa wamemaliza tatizo hilo .

“Mfano wewe ukipokea rushwa na kuamua kufanya tofauti na aliyekuhonga kwa kuwa baadaye atakuwa hajapata kile alichotaka kukinunua toka kwako, unafikiri kesho atarudia”.

Vijana.
Amewataka vijana nchini kupigania maslahi yao kwa mtazamo hasi wenye kuleta mstakabali mzuri wa Taifa, badala ya kufikiri kuwa mabadiliko ni kuiondoa CCM madarakani na kuiweka Chadema.

Alisema kuna mambo mengi ya msingi ambayo kama vinana wanapaswa kuwahoji viongozi waliowachagua kama wameyatekeleeza , ikiwemo kupigania katiba mpya kuwa na sera ya inayoweza kuruhusu mgombea binafsi kwa kuwa huko wanaweza kupata viongozi bora.

Kujiengua kwa Nyimbo linaweza kuwa ni pigo kubwa kwa Chadema, kwani baada ya kujiunga na chama hicho mwaka 2010, alikuwa ni mlezi wa Chadema kwa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, huku pia akiwa ni miongoni mwa wanasiasa wenye mvuto na wahamasishaji wazuri wa Chadema katika mkoa mpya wa Njombe.

Habari kwa hisani ya Moses Ng’wat,Mbeya. picha na Mbeya yetu