WAPENDEKEZA MAWAZIRI WASIWE WABUNGE, VITI MAALUMU VIFUTWE, URAIS MIAKA 35
WABUNGE jana walijilipua baada ya baadhi yao
kupendekeza kuwa muundo wa Muungano ubadilishwe kuwa wa Serikali tatu na
kwamba, mawaziri wasiwe wabunge.
Pamoja na mapendekezo hayo, wengine walitaka umri wa kugombea urais ushushwe na kuwa miaka 35, badala ya sasa ya miaka 45.
Wakitoa maoni yao kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba mjini Dodoma jana, wabunge hao pia
walitaka viti maalumu vya ubunge vifutwe, badala yake wanawake warejee
kugombea ubunge majimboni.
Katika mkutano huo, zaidi ya wabunge 36 walitumia
nafasi hiyo kutoa maoni yao kuhusu masuala mbalimbali yenye masilahi kwa
taifa, waliyoona yanafaa kuingizwa kwenye Katiba Mpya, ambayo mchakato
wa ukusanyaji maoni ya uundwaji wake, unaendelea.
Muungano
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alitaka muundo wa muungano ubadilishwe na kuwa wa Serikali tatu, badala ya uliopo sasa aliosema una kasoro nyingi.
Moja ya kasoro hiyo ni wawakilishi kuruhusiwa
kuingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano, huku wabunge wa Bara wakiwa
hawana uwakilishi katika Baraza la Wawakilishi.
“Mwenyekiti, tuwe na Serikali tatu katika muungano, vinginevyo kila mmoja abaki na chake," alisema.
“Mwenyekiti, tuwe na Serikali tatu katika muungano, vinginevyo kila mmoja abaki na chake," alisema.
Pia alitaka viti maalumu vifutwe, badala yake wanawake wawekewe majimbo ya wilaya, ambayo watagombea na wenzao.
Mbunge wa Kilindi (CCM), Beatrice Shelukindo naye
alitaka muundo wa muungano uwe wa Serikali tatu pamoja na kuruhusiwa kwa
mgombea binafsi katika nafasi mbalimbali.
Alisema kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa
wilaya wasitokane na wabunge kwa sababu hawataweza kufanya kazi kwa
ufanisi na ni mgongano wa kimasilahi.
Mbunge wa Mkanyangeni (CUF), Mohamed Mnyaa alitaka kuwapo na Serikali tatu katika muungano.
Mbunge wa Mkanyangeni (CUF), Mohamed Mnyaa alitaka kuwapo na Serikali tatu katika muungano.
Alisema kama Tanzania Bara watakataa kuita nchi yao Tanganyika basi wanaweza kuiita jina lolote hata Mzizima.
“Muungano uwe wa Serikali tatu, Tanganyika wawe na
nchi yao na sisi tuwe na Zanzibar yetu, kama bara hawataki kuiita nchi
yao Tanganyika basi wanaweza kuiita hata Mzizima,” alisema.
Kwa upande wake Mbunge wa Chakechake, (CUF), Mussa
Haji Kombo alitaka muundo wa Muungano uliopo ubadilishwe badala yake
uwe wa mkataba.
Alisema muundo uliopo hivi sasa unawanyima haki Wazanzibar,
akitoa mfano wa suala la mafuta alilosema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
(SMZ), haina uwezo wa kufaidi raslimali yake bila ya kuwasiliana na
Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
“Tuvunje muungano huu, tuanzishe ushirikiano mpya wa mkataba,” alisema.
Mawaziri
Akitoa maoni yake, Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-
Mageuzi) Moses Machali alisema kuwa mawaziri wasiwe wabunge ili kuondoa
mgongano wa kimasilahi.
Alisema kuwa ni vigumu kwa wabunge kumdhibiti waziri ambaye ni mbunge mwenzao kama ilivyo sasa.
Alisema kuwa ni vigumu kwa wabunge kumdhibiti waziri ambaye ni mbunge mwenzao kama ilivyo sasa.
Alipendekeza kuwa, Katiba Mpya itamke kuwa mtu
akipatikana na kosa la kuhujumu nchi anyongwe pamoja na kuwapo kwa
Serikali ya Majimbo, ambayo itasaidia Serikali kutoa huduma kwa
wananchi.
Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Kessy
alitaka umri wa mtu kuruhusiwa kugombea urais upunguzwe kutoka miaka 45
ya sasa hadi miaka 35.
Alisema kuwa umri huo utasaidia kupatikana rais
kijana, ambaye anaweza kuhimili vishindo kwa kutembea mikoani bila ya
kuchoka, badala ya kuwa na rais mzee atayekuwa akienda kutibiwa nchini
India mara kwa mara.
Mbunge huyo alipendekeza pia wabunge wawe na
kikomo kwa kutumikia vipindi viwili na kwamba, viongozi wastaafu
wasiruhusiwe kuwapo bungeni akieleza kuwa hivi sasa wengi wanatumia muda
mwingi kusinzia.
Kessy alipendekeza pia Baraza la Mawaziri lipunguzwe ukubwa akitaka wawe mawaziri 14 na manaibu mawaziri wawe 24.
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter
Msigwa, alitaka kuwapo Tume Huru ya Uchaguzi na mwenyekiti wake
akiteuliwa na Rais, lakini athibitishwe na Bunge.
Pia alitaka viti maalumu vya ubunge vifutwe na badala yake wanawake waende katika majimbo kugombea sambamba na wanaume.
Pia alitaka viti maalumu vya ubunge vifutwe na badala yake wanawake waende katika majimbo kugombea sambamba na wanaume.
Msigwa alisema kuwa kuendelea kuwa na wabunge wa
viti maalumu ni kuwafanya waendelee kujiona wanyonge, wakati hivi sasa
kuna wanawake wenye uwezo mkubwa sawa na wanaume.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Zakia Meghji alitaka
muundo wa muungano uliopo ubaki kama ulivyo isipokuwa kero ndogondogo
za muungano ziondolewe.
Alisema suala la uchumi wa Zanzibar linatakiwa kuangaliwa upya ili kuwafanya Wazanzibar kunufaika na raslimali zao.
Alisema suala la uchumi wa Zanzibar linatakiwa kuangaliwa upya ili kuwafanya Wazanzibar kunufaika na raslimali zao.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe
alisema muundo wa muungano ubadilishwe kuwe na rais mmoja na mawaziri
wakuu wawili wa kutoka Zanzibar na Bara.
Alipendekeza Rais akae madarakani kwa kipindi cha miaka saba na baada ya hapo asiruhusiwe kugombea tena.
CHANZO: MWANANCHI
Alipendekeza Rais akae madarakani kwa kipindi cha miaka saba na baada ya hapo asiruhusiwe kugombea tena.
Zitto pia alizungumzia umri wa kugombea urais akitaka uwe miaka 35 na kwamba wanaotaka umri wa miaka 45 hawana hoja.
Mbunge huyo amekuwa akikaririwa akitaka umri wa
urais uwe miaka 35, akisema anaweza kugombea urais katika uchaguzi mkuu
ujao wa mwaka 2015.
Kauli hiyo imekuwa ikimletea mgogoro mkubwa kati yake na viongozi wa chama chake akiwamo mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei.
Mbunge wa Tarime (CCM), Nyambari Nyangwine alitaka
umri wa kugombea urais uwe miaka 35, ili kutoa nafasi kwa vijana
kushika nyadhifa za juu za uongozi wa nchi.
Pia alitaka Kiswahili kiwe lugha rasmi na kwamba mikataba yote muhimu ya uwekezaji isainiwe bungeni.
Pia alitaka Kiswahili kiwe lugha rasmi na kwamba mikataba yote muhimu ya uwekezaji isainiwe bungeni.
Nyangwine alitaka Katiba Mpya itamke kuwa watu wanaopatikana na makosa ya kuhujumu nchi wanyongwe.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment