Baadhi
ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wametaka Katiba mpya iwe na
kipengele ambacho kitaondoa matabaka katika kutoa mikopo kwa wanafunzi
wa elimu ya juu.
Waliyasema hayo jana wakati wakitoa maoni ya katiba.
Juliana Ng`onda, alisema kama serikali inataka kutoa kipaumbele katika sekta ya elimu ni vema katiba mpya ikaondoa kipengele cha kutoa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa kufuata ufaulu wao.
“Ninaomba katiba mpya itamke kwamba mikopo kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu isitolewe kwa kufuata ufaulu wao bali iwe inatolewa sawa kwa kila mwanafunzi mwenye sifa ya kujinga na elimu ya juu,” alisema.
Juma Hassan, alisema: “Endapo katiba mpya itatamka hivyo, idadi kubwa ya wanafunzi hususani wanaotoka katika familia maskini watapata fursa ya kuendelea na masomo.”
Hassan alisema asilimia kubwa ya wanafunzi wanaotoka katika familia duni hushindwa kuendelea na elimu ya juu kutokana na kukosa ada.
“Wanafunzi wa wanaotoka katika familia duni wanasoma katika mazingira magumu sana, hivyo kupata alama ya juu ya kuwawezesha wapewe mkopo kama wale wanaotoka katika familia zenye uwezo mkubwa ambao wengi wao hufaulu vizuri,” alisema na kuongeza
“Sio rahisi, lakini ukifuatwa utaratibu wa kutoa mikopo hiyo kufuatana na ufaulu, watawakomboa.”
Waliyasema hayo jana wakati wakitoa maoni ya katiba.
Juliana Ng`onda, alisema kama serikali inataka kutoa kipaumbele katika sekta ya elimu ni vema katiba mpya ikaondoa kipengele cha kutoa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa kufuata ufaulu wao.
“Ninaomba katiba mpya itamke kwamba mikopo kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu isitolewe kwa kufuata ufaulu wao bali iwe inatolewa sawa kwa kila mwanafunzi mwenye sifa ya kujinga na elimu ya juu,” alisema.
Juma Hassan, alisema: “Endapo katiba mpya itatamka hivyo, idadi kubwa ya wanafunzi hususani wanaotoka katika familia maskini watapata fursa ya kuendelea na masomo.”
Hassan alisema asilimia kubwa ya wanafunzi wanaotoka katika familia duni hushindwa kuendelea na elimu ya juu kutokana na kukosa ada.
“Wanafunzi wa wanaotoka katika familia duni wanasoma katika mazingira magumu sana, hivyo kupata alama ya juu ya kuwawezesha wapewe mkopo kama wale wanaotoka katika familia zenye uwezo mkubwa ambao wengi wao hufaulu vizuri,” alisema na kuongeza
“Sio rahisi, lakini ukifuatwa utaratibu wa kutoa mikopo hiyo kufuatana na ufaulu, watawakomboa.”
CHANZO: NIPASHE



No comments:
Post a Comment