HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » YALIYOJILI KWENYE MCHEZO WA STARS ILIVYOICHAPA ZAMBIA 1-0

 Mshambuliaji wa Taifa Stars,Hamis Mcha (katikati) akiwachachafya mabeki wa timu ya Zambia katika mchezo wa kirafiki uliomalizika muda mfupi uliopita kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Taifa stars imeshinda goli 1-0.
 
 Hamis Mcha (7) akiendelea kuwapa kazi mabeki wa timu ya Zambia.
 
 Mchezaji wa timu ya Zambia, Moses Phiri (9) akiingia kwenye lango la timu ya Taifa Stas,huku beki wa Stars,Aggrey Moris akijiandaa kukabiliana nae.
 Mchezaji wa timu ya Zambia,Moses Phiri (9) akijipinda kumramba chenga Kiungo wa Stars, Salum Abubakar, kutaka kumtoka wakati wa Mchezo wa Kirafiki wa Kimataifa uliochezwa leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar.
 Hii ni Nduki aliyoipiga Mrisho Ngassa na kuingia wavuni moja kwa moja huku kipa wa timu ya Zambia Chipolopolo, Danny Munyao akiwa hana la kufanya na kuishia kuutizama ukijaa wavuni.
 Hili ndilo goli la Mrisho Ngassa , Mpira ukijaa wavuni
 Baada ya kufunga goli alianza kwa kushangilia kwa namna hii kama anavyoonekana katika picha
 Hii ni sehemu ya pili katika kushangilia
 Sehemu ya tatu akipiga saluti yote hiyo ni katika mwendelezo wa kushangilia
Baada ya furaha aliamua kumbeba, Ari Kiemba badala ya kubebwa yeye
Mashabiki wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars wakiwa na nyuso za furaha baada ya Taifa Stars kuibuka na ushindi wa bao 1-0,  dhidi ya Zambia.

Baada ya furaha aliamua kumbeba, Ari Kiemba badala ya kubebwa yeyeKatika mchezo huo, Taifa stars imeibuka ushindi wa bao 1-0,  lililotiwa kimiani na Mshambuliaji machachaari, 'Kisirani' Mrisho Ngassa katika dakika ya 45 ya kipindi ca kwanza.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: