Taarifa lizizotufikia hivi punde zinasema kuna Jengo jipya lililokuwa
linajengwa limeporomoka na kuangukia msikiti (kama inavyoonekana
pichani) asubuhi hii mwendo wa saa mbili na nusu, katikati ya jiji la Dar
es Salaam, kwenye barabara ya Mororogo. Kilicho kuwa
kituo cha mabasi ya Sinza zamani uko posta, mtaa wa Hindi Ragani na yapata watu
60 takribani kuwa ndani ya poromoko ilo, na pamoja walio kuwa karibu ya jengo
,wakiwemo na hawa omba omba.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo
kutoka kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (CP),
Suleima Kova kuhusu jengo la ghorofa 16 lililoanguka majira ya saa mbili
asubuhi katika makutano ya mtaa wa Indira Ghandi na Barabara ya
Morogoro jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala,
Marietha Minangi. Katika ajali hiyo watu wawili wamekufa papo hapo.
(Picha zote na Habari Mseto Blog)
Hizi nia aina ya nondo ambazo kimsingi sio imara kuweza kuhimili ujenzi wa ghorofa ndefu kama hili, kuna haja mamlaka husika likatupia macho kampuni za ujenzi ili kuokoa maisha ya wajenzi na watumiaji wa majengo hayo.



No comments:
Post a Comment