AJALI MBAYA YATOKEA MUDA HUU ILALA BOMA NA KUSABABISHA KIFO CHA MTU MMOJA

Asubuhi hii ajali mbaya imetokea maeneo ya Ilala Boma na  kusababisha kifo cha abiria huyu ambaye hajatambulika kwa jina mpaka sasa baada ya abiria kutaka kudandia bahati mbaya akadondoka na kupasuka kichwa na kusababisha umauti wake
Wasamaria wema wakisaidia kumpakia kwenye gari kwa kumpeleka hospitalini
Damu ya marehemu ambayo kwa kiasi kikubwa imetoka kichwani baada  ya kupasuka vibaya
Mwili wa marehemu ukiwa tayari kuondolewa kwenda hospitali
Hii ndio daladala ambayo marehemu alikuwa akitaka kudandia na kudondoka kwa bahati mbaya

Umati wa watu ukishuhudia ajali maeneo ya Ilala Boma asubuhi hii
Askari wa usalama barabarani akichukua maelezo kwa dereva aliyesababisha ajali



PICHA ZOTE NA KRANTZ MWANTEPELE

No comments

Powered by Blogger.