Mshambuliaji wa Napoli na Timu ya Taifa ya Uruguay, Edinson Cavanni
KLABU za Chelsea na Manchester City
zitalazimika kuvunja rekodi ya dau la usajili Uingereza kama zinataka
kumsaini mshambuliaji wa Napoli, Edinson Cavanni baada ya matajiri wa
Ufaransa, Paris Saint-Germain kutoa ofa ya Pauni Milioni 43 kwa nyota
huyo wa Uruguay.
Endelea kusoma habari hii kwa kubofya hapa chini
Cavani anatakiwa na klabu zote,
Chelsea na City, lakini dau la PSG linamaanisha watatakiwa kupanda ili
kilipiku ndipo wampate mshambuliaji huyo.
Dau la PSG linakaribia Pauni Milioni 53.9, ambazo Napoli inataka ambazo zitahusu pia kodi wa dili hilo.
Real Madrid bado haijafika bei na Cavani alisema wiki iliyopita kwamba tetesi zimezidi kuhusu hatima yake.
"Mwanzoni mwa Kombe la Mabara,
sikuamini kwamba tetesi za usajili zingenisababishia matatizo. Lakini,
mwishoni, nakubali wananisumbua kidogo,"alisema.
Chelsea inashikilia rekodi ya kusajili
kwa bei chafu Uingereza, Pauni Milioni 50 walizotoa kumsaini Fernando
Torres, Januari 2011.





No comments:
Post a Comment