HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » YALIYOJIRI LEO KWENYE ZIARA YA RAIS OBAMA MPAKA KUONDOKA KWAKE

 
Ndege aina ya "Airforce one" iliyombeba Rais wa Marekani, Barack Obama ikiwa angani kuelekea Marekani
Msafara wa Rais Barack Obama ukiwa maeneo ya Mwenge ukielekea Ubungo



Endelea kutizama tukio hili kwa kubofya hapa chini

Msafara wa Rais Barack Obama ukielekea Ubungo

Gari ya Rais wa Marekani Barrack Obama,ikiingiaka kwenye kiwanda cha kufua umeme cha Symbion eneo la Ubungo kabla ya kuelekea uwanja wa ndege

 


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulishaWaziri wa Uchukuzi Mh. Mwakyembe kwa Rais Barrack Obama wa Marekani leo Ubungo
 Rais Barrack Obama wa Marekani na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete  wakizungumza na watendaji wa kuu wa sekta ya umeme nchini.Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mr.Maswi,mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Sadik Meck Sadik na watatu kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa  Sospeter  Muhongo wakati kiongozi huyo wa Marekani alipotembelea mradi wa kuzalisha umeme unaofanywa na kampuni ya Symbion power ya Marekani huko Ubungo jijini Dar es Salaam leo.

 
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na mwenyeji wake Rais Barrack Obama wa Marekani wakipata maelezo juu ya kituo cha uzalishaji wa Umeme Ubungo kinachoendeshwa na kampuni ya symbion power wakati viongozi hao walipofanya ziara katika kituo hicho leo asubuhi.Watatu kushoto ni Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Symbion Power Bwana
 Waendelea kumsikiliza msemaji wa kampuni ya symbion power
 Rais wa Marekani, Barack Obama akionesha kipaji chake kwenye kituo cha uzalishaji wa Umeme Ubungo leo
Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete(kulia) alishindwa kujizuia nae akaanza kucheza mpira na Rais wa Marekani, Barack Obama kwenye  kituo cha uzalishaji wa Umeme Ubungo
 Gari ya Rais wa Marekani Barrack Obama,ikitoka kwenye kituo cha uzalishaji wa Umeme Ubungo na kuelekea uwanja wa ndege cha Mwalimu Nyerere
Msafara wa Rais Barack Obama ukiwa maeneo ya Buguruni ukielekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere

 Msafara wa Rais Barack Obama ukiwa maeneo ya TAZARA kwenye mataa ukielekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere
 Hili ndilo gari alilokuwa amepanda Rais wa Marekani, Barack Obama wakati anaelekea uwanja wa ndege
 Akiwa anaelekea Airport tayari kwa safari ya kurudi Marekani
Rais Barack Obama wa Marekani ameondoka nchini mchana huu kurudi nchini Marekani, baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili hapa nchini iliyoanza jana

 Rais Obama na mkewe wakikwea pipa lao la Air Force One
 Rais Obama na mkewe wakipunga mikono kuaga Watanzania
 Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiaga wageni wao

 Rais Barrack Obama wa Marekani na mke wake Michelle Obama wakiwaaga watanzania leo kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Adam Malima (kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Balozi wa Marekani hapa nchini Mhe  Alfonso Lenhardt wakipungia kuaga wageni wao
 


PICHA ZOTE NI KWA HISANI YA FULL SHANGWE, GPL, ISSA MICHUZI NA YAHOO

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: