HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » WANAWAKE WALIOMUUNGA MKONO MORSI WAACHILIWA

Mahakama ya rufaa nchini Misri imeamuru kuachiliwa huru kwa wanawake, 21 wakiwemo wasichana saba waliofungwa jela mwezi jana kwa kuandaa maandamano ya kumuunga mkono aliyekuwa Rais Mohammed Morsi.
Watoto hao wamepewa kifungo cha nje cha miezi mitatu. Mahakama hiyo pia ilipunguza kifungo cha miaka 11 walichokuwa wamepewa wanawake hao 14.
Mahakama iliwapata na hatia mwezi jana ya kuwa sehemu ya kundi la kigaidi lililokuwa linatatiza usafiri wa magari, kufanya hujuma na kutumia nguvu kufanya vitendo vyao.
Hata hivyo makundi ya kutetea haki za binadamu yamekosoa hukumu hiyo.
Mmoja wa wanaharakati hao walitaja hukumu hiyo kama ya wazimu.
Wanawake hao walifikishwa mahakamani wakiwa wamevalia nguo nyeupe huku wakiwa wamebeba maua ya waridi.

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

Aidha wanawake hao na watoto walishiriki maandamano ya kumuunga mkono aliyekuwa rais Morsi na jamaa zao wanasema ni maandamano ya kwanza waliyowahi kushiriki na kuyaendesha bila vurugu.
Mamia ya watu wameuawa nchini Misri tangu hatua ya kumwondoa Morsi mamlakani mwezi Julai kusababisha maandamano na vurugu nyingi.

BBC SWAHILI

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: