HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » WATANZANIA, WAKENYA WATOSHANA NGUVU UHURU MARATHON


 Mshindi wa Kwanza wa Mbio ndefu za KM 42 katika Mashindano ya Uhuru Marathon,Jamin Ikai (kutoka nchini Kenya) akiwasili kwenye viwanja vya Leaders Club wakati akimaliza mbio hizo,zilizofanyika leo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania.
 Mshindi wa Kwanza wa Mbio ndefu za KM 42 katika Mashindano ya Uhuru Marathon, Jamin Ikai akishangilia ushindi wake huo leo.
Mshindi wa Tatu wa Mbio fupo za KM 21,Elia Daud akishangilia wakati akimaliza mbio hizo.

ENDELEA KUTIZAMA TUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI


 Washindi wa Mbio ndefu za KM 42 katika Mashindano ya Uhuru Marathon wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi,mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.Mshindi wa Kwanza ni Jamin Ikai (kutoka Kenya),Steven Selevestor (kutoka Jeshi la Magereza Tanzania) pamoja na Aley Sanka (Tanzania).
 Washindi wa Mbio ndefu za KM 42 (wanawake) wakiwa wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi,mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.Mshindi wa wa Kwanza ni Thabita Kibet (kutoka Kenya),Naum Jerkosgei (Kenya) pamoja na Banoela Brigton.
 Washindi wa Mbio fupi za KM 21 (wanaume) wakiwa wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi,mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.Mshindi wa Kwanza ni Aliya Tirot (Kenya),Wilson Titoe (Kenya) pamoja na Elia Daud.
 Washindi wa Mbio fupi za KM 21 (wanawake) wakiwa wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi,mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.
 Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Mbio za Uhuru Marathon,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na Mratibu wa Mbio hizo za Uhuru Marathon,Innocent Melleck wakati akiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenella Mukangara.
 Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Mbio za Uhuru Marathon,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa hotuba yake wakati wa maadhimisho mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania. 
 Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenella Mukangara akisoma hotuba yake kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi,wakati wa maadhimisho mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania. 
 Mkuu wa Wilaya Temeke,Mh. Sophia Mjema akizungumza wakati wa maadhimisho ya mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania. 
 Mratibu wa Mbio za Uhuru Marathon,Innocent Melleck akizungumza wakati wa maadhimisho ya mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania. 

 Wadau mbali mbali wakati kwenye maadhimisho ya mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania. 
 Mmoja wa washiriki wa mbioa hizo akitoa salamu ya Kijeshi kwa Makamu wa Rais.
 Washiriki Mbali mbali wa Mbio za Uhuru Marathon wakimaliza mbio hizo. 
 Wadau.
 Ankal Hashim Lundenga pia alishiriki mbio hizo.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: