HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » UTAFITI: WATOTO HAWA HAWAWEZI KUUGUA UKIMWI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Uchunguzi uliofanywa na wanasayansi wa chuo cha Oxford umeonyesha kuwa asilimia 10 ya watoto walioambukizwa virusi vya HIV hawapati ugonjwa wa Ukimwi licha ya kutopata matibabu.
Utafiti uliofanyiwa watoto 170 walio na virusi vya HIV nchini Sudan Kusini ulionyesha kuwa kinga yao ya mwili ililingana na ya nyani waliokuwa na virusi hivyo.
Wataalamu wanasema kuwa ugunduzi huo ni ishara ya kwanza ya watu wanoishi na virusi vya HIV, ambao utasababisha kupatikana na tiba kwa wagonjwa wote walio na virusi hivyo.
Ikiwa virusi vya HIV haviwezi kutibiwa vinaweza kuwaua asilimia 60 ya watoto walio na virusi hivyo katika kipindi cha miaka miwili unusu.
Kisha virusi hivyo huua kinga yote ya mwili na kuacha mwiwi kwenye hatari ya kuambukizwa maradhi mengine.
Watafiti walichunguza damu kutoka kwa watoto 170 kutoka Sudan Kusini waliokuwa na virusi vya HIV, ambao hawakupata matibabu na ambao hado hawakuwa wameugua ugonjwa wa ukimwi.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: