HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » RAHCO: Bomoabomoa Moshi, Tanga iko palepale

Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (Rahco) imesema bomoabomoa ya nyumba zilizopo katika hifadhi ya reli (mita 30 kila upande) iko palepale tofauti na ilivyoelezwa kwamba kwenye baadhi ya mikoa itakuwa tofauti.
Septemba 29 mwaka huu ofisa habari wa kampuni hiyo, Catherine Moshi aliiambia Mwananchi hili kuwa katika mkoa wa Kilimanjaro, Tanga na Dar es Salaam watalegeza masharti ya umbali kwa majengo yanayopaswa kubomolewa
Leo Jumatano katika tangazo lao lililotolewa katika gazeti la Mwananchi, Rahco imesema itaendelea na zoezi la kuwaondoa wavamizi wote wa hifadhi za reli nchi nzima, waliopewa notisi na kuwekewa alama ya X.
“Rahco inakanusha uzushi unaoenezwa kuwa kuna mabadiliko ya upana katika hifadhi ya reli kwa baadhi ya mikoa,” limeeleza tangazo hilo.

Chanzo: Mwananchi

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: