Ili mtoto akue akiwa na afya bora na isiyo na mgogoro basi anatakiwa
apate chanjo zote muhimu za utotoni ambazo ndio msingi mkuu wa kuzuia
vifo vingi vya watoto, ukuaji mzuri na kuzuia kudumaa.
Kumekua na imani potofu kuhusu chanjo za watoto na kuna baadhi ya wazazi
hawawapeleki kabisa watoto wao kupata chanjo hata kama zinapatikana
karibu yao, na kitu kinachoshangaza zaidi chanjo hizi hutolewa bure
kabisa bila malipo yeyote hivyo ni jukumu la mzazi kuhakikisha mwanae
kapata chanjo zote kwa kukagua kadi yake ya kliniki.
Zifuatazo ni chanjo ambazo mtoto anatakiwa azipate zote kwa muongozo wa hapa Tanzania
Siku ya kuzaliwa; hii ni siku mtoto anatoka tumboni mwa mama
yake, siku hii mtoto anatakiwa apate chanjo ya kifua kikuu kitaalamu
kama bcg ambayo inachomwa kwenye bega la kulia chini kidogo ya ngozi kwa
kiasi cha 0.05mils, kimsingi chanjo hii inatakiwa iache kovu..pia siku
hii mtoto anapewa matone mawili mdomoni kuzuia ugonjwa wa polio ambao ni
ugonjwa wa kupooza miguu yote miwili na huleta kilema cha maisha.
Baada ya wiki sita; baada ya wiki ya sita baada ya kuzaliwa
mtoto anapewa chanjo ya pili ya polio matone mawili mdomoni, anachomwa
chanjo ya pentavalent 1 paja la kushoto ambayo inazuia magonjwa matatu
yaani tetenasi[ugonjwa wa mishipa ya fahamu], donda koo[ugonjwa wa koo]
na kifaduro[ugonjwa wa mfumo wa hewa]
lakini pia siku hii mtoto huchomwa chanjo ya pcv kwenye paja la kulia
kuzuia ugonjwa wa kichomi kitaalamu kama pneumonia ambao ni moja ya
magonjwa yanayoua sana baada ya malaria kwa hapa tanzania na mwisho
kabisa mtoto hupewa chanjo ya kunywa kitaalamu kama rotal inayozuia
kuharisha ambako kunasababishwa na virusi vya rota virus.
Wiki ya kumi: wiki ya kumi mtoto hupata chanjo zote ambazo
nimezitaja kwenye wiki ya sita yaani kwa awamu ya pili kwa mtiririko
uleule bila kuruka chanjo hata moja.
Wiki ya kumi na na nne; kipindi hiki mtoto hupata chanjo za
marudio lakini baadhi ya chanjo alizochoma wiki ya sita na kumi hupungua
hivyo wakati huu hupata chanjo ya polio ya mdomoni, pentavalent ya
kuchoma paja la kushoto na pcv ambayo huchomwa paja la kulia.[kazi zake
nimezielezea kwenye wiki ya sita.
Mwezi wa tisa; kwa mpangilio wa chanzo za nchini tanzania hii
ndio chanjo ya mwisho kabisa ya ugonjwa wa surua ambayo inachomwa kwenye
mkono wa kushoto.
mwisho;kuna watafiti wamegundua chanjo ya malaria na wanategemea
kuanza kuitoa mwaka 2017 na kuisambaza chini ya jangwa la sahara, huenda
ikawa ndio mwisho wa vifo vya malaria kwa nchi nyingi zilizo athirika.
IMEANDALIWA NA DOCTOR JOH BLOG
No comments:
Post a Comment