Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Wanadamu wote tumeumbwa na kupewa akili ambayo inabidi tuitumie vizuri ili kuweza kuishi vyema katika ulimwengu huu. kinachoshangaza ni kwamba wapo watu wachache tu ambao wamekuwa wakitumia akili vizuri na kufanya vitu vikubwa vinavyo wapatia mafanikio makubwa, huku wengi wetu tukiwa tumebaki kusema kuwa wao wamebahatika.
Hakuna watu waliozaliwa na bahati au mikosi, wanadamu wote
wanauwezo wakutumia akili vizuri na kujipatia kipato kikubwa sana. yapo mambo
kadha wa kadha ambayo inabidi tuweze kuyafanya ili kuhakikisha kuwa tunasonga
mbele na kuwa na maisha mazuri.
Umakini na nidhamu. nidhamu inachukua sehemu kubwa sana kuliko unavyoweza kufikiria.
hakikisha unakuwa na ratiba inayoeleweka ambayo itakuwa inakuongoza katika
shughuli zako za kila siku. hii itaongeza ufanisi, lakini pia nidhamu humfanya
mtu aheshimike na kuoneka ana thamani katika jamii, kitu kinachoweza kufanya
watu wakupatie kazi mbalimbali kwakuwa wanaamini hauta waaibisha.
Dhamira. uaminifu umekuwa adimu sana kwa watu wengi, jambo linalopelekea
watu kukosa nafasi mbalimbali kwakuhofiwa kufanya ubadhilifu. ukiwa mwaminifu
ni rahisi kupata fursa nyingi na kazi nzuri zenye maslahi mazuri. uaminifu ni
silaha kubawa sana katika maisha.watu waliofanikiwa walikuwa waaminifu kwa
sehemu kubwa, hawakuwa na tamaa ndogondogo zisizo nafaida. hakuna haja ya kuiba
fedha kidogo ambazo zitachafua jina lako na kufanya heshima yako ipotee.
kumbuka kuwa ni rahisi sana kupoteza heshima kuliko kuijenga.
Usiwe na matumizi yasiyo na msingi. watu wengi hawafanikiwi
kwasababu wanatamani maisha ya wenzao, wanapenda waonekane wana maisha ya juu
wakati sio kweli. hakuna haja ya kutafuta sifa mbele za watu wakati ukirudi
kwako unaanza kujuta kwa matumizi uliyoyafanya. weka akiba kwa kile
unachokipata, achana na starehe zisizo za msingi. unywaji wa pombe unafilisi
sana na unakwamisha sana maendeleo ya watu wengi. ishi maisha yaliyo ndani ya
uwezo wako, ukiwaza kupiga hatua na si kudumaa hapohapo ulipo.
Fanya kazi kwa bidii na kwa malengo ili uwe na maisha mazuri. uvivu wa kufikiri na wa kufanya kazi unakwamisha maendeleo. tazama
watu wote waliofanikiwa wanafanya sana kazi kwa bidii. Mwenyezi Mungu alisema
kuwa asiyefanya kazi na asile, usichague kazi ya kufanya ilimradi isiwe
inavunja sheria. tuache ubishoo wakuona kuwa kuna kazi ambazo hazikustahili
wakati huna kazi ya kufanya.
Kuwa mbunifu, lakini pia tumia kipaji chako
kujipatia kipato. usijilinganishe maisha yako na yawatu wengine, usiangalie
watu waliofanikiwa bali angalia watu walio chini yako. mshukuru Mungu kwa uhai
na uzima ulio nao. Fanya kazi kwa bidii ukimtanguliza Mungu utafanikiwa tu.
No comments:
Post a Comment