HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » PENZI LA SHEMEJI SEHEMU YA HAMSINI NA NNE (54)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



Joan alishtuka sana kumkuta Shemeji akiwa pale sebuleni katulia na wala hana tatizo la kuonesha kuna tukio limemkuta " Vip? Mbona umeshtuka hivyo?" akauliza shemeji " Aaaaaaah! Hap...hapana,ila nashangaa umefikaje hapa? Na umeingiaje?" akasema kwa uwoga wa dhahiri Joan " Usijal hapa ni kwangu najua niingieje na sipangiwi muda wa kurudi" akajibu " Kalibu dada,za huko lakin?" akauliza Joan " Achana na mimi kwanza,huyu nyang'au kaenda wap?" akauliza " sijui dada" akajibu " Hujui eee? Unafikiri sijui kinachoendelea? 
Sasa subiri dawa iko jikoni inachemka,naona watu wana bep kifo hapa ndani" akasema " Sikuelewi dada" akasema Joan " Utanielewa tu siku ukiona mtu anakata roho mbele yako,wewe si hunielew? Subir" akajibu " Mtu nipo matatizoni,jana angewekwa yeye selo ila nikamuonea huruma anakuja kunifanyia mimi uhuni? Hamnijui nyie,mimi ni mhuni wa wahuni,kama jambazi basi mimi ndo mkuu wao,na lazima mtu alambe udongo hapa ndani" aliendelea kufoka " 
Sasa sikia mimi natoka ila mwambie huyo nyang'au kuwa hapa ndani ili aman irudi lazima mtu alambe ardhi hapa" akasema kwa vitisho na kuondoka Aliondoka na kutoka nje ya geti,Joan hakutaka kuamin kuwa kaondoka ilimbidi kwenda mpaka getini ndipo akaona gari ikipotelea mbali na upeo wa macho yake Alipohakikisha keshapotelea mbali alirudi ndani speed mpaka chumbani na kuanza kuniamsha kwa fujo " Wewe,,,amka,,Jun amka kuna matatizo" akasema " Wewe nini unanisumbua?" nikauliza " 

Please Jun amka mimi nakufa jaman,mama yangu marehemu nakufa bado mtoto mdogo kwa tamaa za kijinga mimi" aliongea kwa uchungu mpaka akaanza kulia Kile kilio chake namaneno yakanishtua ikabidi niamke na kupikicha macho yangu kuondoa usingizi " Kuna nini? Mbona unalia tu bila mpango hapa? Tlia sasa unieleze" nikamwambia " Jun umeniponza mwenzako jaman,kwanini lakin? 
Nakufa najiona jaman eeee baba yangu nisaidie jaman" aliendelea kulia Wakati anaendelea kulia simu yake iliyokuwa kwenye stuli ya pale chumbani ikaanza kuita Hakujali kujishughulisha nayo ila mimi niliitupia jicho na kuona jina la mpigaji " Shemejiiiiiii???????? Mmmmmmh!" nilishtuka sana kwa sababu mpaka muda huo nilijua yuko ndani na hajatoka 
Aliposikia nimetamka shemeji akashtuka na kuja kuiangalia simu,alipoona jina la dada yake alishtuka sana " Jaman nitamweleza nini mimi? Umeniponza Jun jaman" akasema Alikaa sekunde kadhaa akijalibu kuondoa ile sauti ya kilio ili aongee na dada yake " Haloo dada" akapokea " Uko nyumban?" " Ndiyo dada" " Huyo kenge yupo?" " Hapana dada" Hivi nikuulize ulishawah kuingia chumbani kwangu?" " Sijawahi dada" " Jana usiku ulifata nini kule chumbani?" " Me sijaingia huko" " Nani alibadilsha mashuka yangu na kuweka ya ziada? 
Na yale yalienda wap? " " Sijui dada" " Nikuibie siri?" " Ndiyo" " Jun hajui kutandika kitanda,na ndani kwangu nimekuta damu mbichi na utandikaji wa kile kitanda ni wa mwanamke tena msafi na sio Jun" " Sio....." hakumaliza kuongea simu ikakatika " Nini kinaendelea?" nikamuuliza " Wakati natoka chumbani nimemkuta dada hapo nje,kaniuliza maswali ya ajabu sana,mpaka nilihisi kufa" akajibu " Mama yangu tumekwisha" nikajibu " Na amenambia lazima afe mtu hapa ndani ndiyo aman iwepo,nahisi ataniua mimi ili muishi kwa amani,Jun umeniletea kifo jaman eee baba nisaidie yatima mimi" alilalamika Nilihisi kubanwa na haja ndogo,hasa nilipokumbuka matukio ya mauaji ya shemeji!!

ITAENDELEA JUMATANO

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: