HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » WATU 40 WAFARIKI KUFUATIA GARI LA KUBEBEA MAFUTA KULIPUKA NCHINI KENYA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Lori la mafuta limelipuka nje ya mji wa Nivasha nchini Kenya usiku wa Jumamosi December 10 2016 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40.
Taarifa iliyotolewa mapema leo December 11 2016 asubuhi na msemaji wa idara ya taifa ya mambo ya dharura nchini Kenya Pius Masai amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kwamba magari zaidi ya 11 yameteketezwa kwa moto katika barabara ya Nairobi-Naivasha.
Maafisa kutoka wizara ya usafirishaji wakiongozwa na Katibu mkuu wa wizara hiyo Irungu Nyakera wamewasili katika eneo la tukio na Taarifa zaidi zinaeleza kuwa watu wengi wamejeruhiwa na miongoni mwao ni watu waliokuwa wakirejea nyumbani kutoka harusini subukia.

Katibu mkuu  Irungu amesema kuwa kwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa ajali hiyo imetokana na dereva kutokufahamu vizuri barabara hiyo kutokana na kwamba lori hilo la mafuta ni la nchini Uganda.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: