TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI: LEO NILIPOKWENDA KUMJULIA HALI MTOTO OMBENI MBEULA ALIYEUNGUA NA MOTO HUU NI MWENDELEZO WA HABARI YA JANA
Mtoto Ombeni anakula mwenyewe leo
Leo nilienda kumjulia hali mtoto Ombeni Mbeula ambaye alipata ajari ya moto huko
Mpwapwa. Kikubwa zaidi nimepata taarifa nyingine kuhusu mtoto Ombeni Mbeula
kwamba alifikishwa hospitalini hapo tarehe 14/12/2012 lakini mpaka jana alikuwa bado hajapata matibabu. Mpaka baada ya blog ya PAMOJAPURE kurusha habari kwenye
mtandao na pia mabloger wengine walitumiwa habari kupitia kwenye blog ya
PAMOJAPURE ili aweze kusaidiwa kwa matibabu ndipo madaktari wameanza kumpa tiba
mtoto huyo.
Kiukweli
inasikitisha sana kwa Madaktari wa HOSPITALI YA GENERAL iliyoko mjini Dodoma
kutomtibu mtoto Ombeni Mbeula kwa takribani miezi miwili kwa ukosefu wa pesa
kutoka kwa familia yake. Isitoshe mtoto mwenyewe ana miaka mitano (5) inabidi kiutaratibu
apate matibabu bure, hivi kweli uongozi wa hospitali ya General umelisimamiaje
jambo hili?. Kiukweli inasikitisha kwa madaktari kutomjali mtoto Ombeni Mbeula
mpaka habari iliporushwa kwenye mtandao kupitia BLOG YA PAMOJAPURE na washiriki
wake wa blog nyingine ndipo madaktari walipoanza kuitwa lakini hawajaenda kumtibu mtoto huyo.
Mmiliki wa blog ya PAMOJAPURE akiwa hospitalini kumjulia hali ya mtoto Ombeni
Hapa mtoto akiwa anaendelea kula chakula mwenyewe
Mmiliki wa blog ya PAMOJAPURE akiwa hospitalini kumjulia hali ya mtoto Ombeni hapa alikuwa anamweka mtoto huyo vizuri.
Huyo ndiye mdau mkubwa wa blog ya PAMOJAPURE tulipomtembelea mtoto Ombeni hospitali ya General iliyopo Dodoma Mjini
..................................
Kwa moyo wa dhati tunawashukuru wale wote waliotoa michango yao
kupitia kupitia kwenye namba ya ndugu yake ambayo ni Ekiria Paskali na namba yake ya simu ni 0757
498336
Hawa ni
baadhi ya wale walioguswa na tukio hilo na kutoa mchango wao wa hali na mali
jumla ya michango ni shilingi 421,300 mpaka naondoka hospitalini hapo kuna watu walikuwa bado wanaendelea kuchangia. Kama ulikuwa unataka kumchangia mtoto huyu apate matibabu tuma mchango wako kwa kutumia namba hii 0757 498336 mwenye jina lake ni Ekiria Paskali
PICHA KWA HISANI YA PAMOJAPURE BLOG
Post a Comment