CPWAA KUFUNGA MWAKA NA "KATA KITU CONCERT"

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.

Mfalme wa Crunk, Ilunga Khalifa aka Cpwaa amedai kuwa mwishoni mwa mwaka huu amepanga kushirikiana na wasanii wa hapa nyumbani na kutoka nje ya Tanzania kwa ajili ya kuwapa mashabiki wake burudani ya kufungia mwaka 2014 na ‘Kata Kiu Concert’.

Cpwaa ameuambia mtandao huu kuwa kwenye show hiyo kutakuwepo na red carpet na kwamba fedha itakayopatikana itatumika kununulia madawati na kupeleka katika shule zenye upungufu wa madawati.
Cpwaa amesema kuna wasanii wa nje ambao wameshafanya nao kazi na kuna ngoma amefanya pia na wasanii wa hapa hapa. Kazi mpya za Cpwaa za sasa ni Chereko Chereko na Kata Kiu.

No comments

Powered by Blogger.