Dowans kaa la moto;Mahakama ya Rufani yaiamuru Tanesco kuilipa Dowans fidia
Uamuzi uliotolewa na jopo la majaji
watatu wa Mahakama ya Rufani walikubaliana na hoja za pingamizi la
Wakili wa Dowans, Kennedy Fungamtama, kuwa maombi hayo yaliwasilishwa
nje ya muda.
Dar es Salaam. Kufuatia Mahakama
ya Rufani kutupilia mbali maombi ya Shirika la Umeme Nchini (Tanesco)
kuzuia utekelezaji wa hukumu ya Mahakama Kuu iliyoliamuru liilipe fidia
Kampuni ya Kufua Umeme wa Dharura, Dowans, wananchi wamehoji sababu ya
Serikali kuzembea hadi deni hilo kuongezeka.
Tanesco iliwasilisha katika Mahakama ya Rufani
maombi ya kusimamisha utekelezwaji wa hukumu ya Mahakama Kuu, ikidai
kuwa Dola za Marekani 65 milioni, walizoamriwa na ICC kuilipa Dowans ni
kiasi kikubwa, endapo kitalipwa Tanesco itapata hasara kiuchumi.
Tanesco iliongeza kuwa kama mchakato wa
utekelezaji wa hukumu hiyo utaendelea, utaathiri uwezo wake wa kuzalisha
na kusambaza umeme nchini na hivyo kusababisha tatizo kubwa la ukosefu
wa umeme, ambao utaathiri uchumi wa nchi kwa jumla.
Hata hivyo, wakati hukumu ya sasa inatolewa riba
ya deni hilo imeongezeka hadi kufikia dola 122 milioni ikiwa ni ongezeko
la dola 58 milioni.
Wakizungumzia ongezeko hilo baadhi ya wanasiasa wameilaumu Serikali kwa kuzembea hadi deni hilo kufikia kiasi hicho.
Wakizungumzia ongezeko hilo baadhi ya wanasiasa wameilaumu Serikali kwa kuzembea hadi deni hilo kufikia kiasi hicho.
Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy alisema
kuwa hasara hiyo inatokana na wanasiasa na wataalamu wa Serikali
kulazimisha kuvunjwa kwa mkataba wa Dowans badala ya kusubiri muda wake
uishe.
“Walifanya haraka kuvunja mkataba wakati ilikuwa
imebaki miezi mitatu tu uishe. Kulikuwa na wanasiasa na wataalamu wetu
walioshinikiza mkataba uvunjwe na hayo ndiyo matokeo yake,” alisema
Keissy.
Naye Mbunge wa kuteuliwa na Mwenyekiti wa NCCR-
Mageuzi, James Mbatia ameilaumu Serikali kwa kutokuwa makini inapoingia
mikataba.
“Mambo ya mikataba ni ya kisheria kati ya pande
mbili. Lazima kuwe na umakini, kwanza ujue nia ya kuingia mkataba,
matazamio na faida zake. Lazima pia kuwe na elimu kwa wataalamu wetu,”
alisema Mbatia na kuongeza;
“Hapa Serikali imekosa umakini ndiyo maana
tumeingia kwenye hasara kama hiyo. Kwa sasa siwezi kusema hatua gani
ichukuliwe kwa sababu sijaiona hukumu lakini huo ni uzembe.”
Naye Mbunge wa Lindi Mjini, Salum Barwany alisema hayo ndiyo matokeo ya Serikali kutokuwa makini na mikataba.
Naye Mbunge wa Lindi Mjini, Salum Barwany alisema hayo ndiyo matokeo ya Serikali kutokuwa makini na mikataba.
“Sisi kama wabunge tuliipigia mno kelele Serikali
bungeni na hata Mwenyekiti wetu wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba
alishasema, hakutakuwa na mafanikio hata kama itakata rufaa. Sasa ndiyo
yametokea. Sasa huu ni mzigo watakaobebeshwa wananchi,” alisema Barwany
na kuongeza:
“Kama wabunge tunapendekeza kuwa mikataba kama hiyo ifikishwe bungeni ili tuijadili kuliko kuwaachia tu watalaamu .”
“Kama wabunge tunapendekeza kuwa mikataba kama hiyo ifikishwe bungeni ili tuijadili kuliko kuwaachia tu watalaamu .”
Kwa upande wake wakili na mwanaharakati wa Kituo
cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia alisema kuwa
makosa yalikwishafanyika tangu mwanzo hivyo, Serikali iwawajibishe
walioingia mkataba huo au hata kushauri.
“Makosa yalishafanyika tangu mwanzo, hivyo Serikali iwajibike.
Kinachoniuma mimi ni kodi za wananchi kutumika kulipia deni hilo.
Wanaotakiwa kulipa hapo ni wale waliosaini mkataba huo au hata kushauri,
” alisema Sungusia.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema
alipotafutwa kwa njia ya simu alikuwa mkali na hakutaka kuzungumzia
suala hilo.
“Wewe unataka mimi niseme nini? Kwanza uwe na adabu siyo kuuliza tu maswali. ‘I am not your age mate and I am not responsible to you…. Halafu unasema ‘what is my take… I don’t know,” alisema na kukata simu.
“Wewe unataka mimi niseme nini? Kwanza uwe na adabu siyo kuuliza tu maswali. ‘I am not your age mate and I am not responsible to you…. Halafu unasema ‘what is my take… I don’t know,” alisema na kukata simu.
Licha ya maombi ya Tanesco, Mahakama ya Rufani
katika uamuzi wake uliosomwa Alhamisi wiki hii na Naibu Msajili wa
Mahakama hiyo, Elizabeth Mkwizu, ilitupilia mbali maombi hayo ya Tanesco
na kuiamuru ilipe gharama za shauri hilo.
Katika uamuzi huo uliotolewa na jopo la majaji
watatu wa Mahakama ya Rufani walikubaliana na hoja za pingamizi la
Wakili wa Dowans, Kennedy Fungamtama, kuwa maombi hayo yaliwasilishwa
nje ya muda.
Wakili Fungamtama katika hoja zake za pingamizi
alidai kuwa maombi hayo yamewasilishwa nje ya muda kisheria. Alidai kuwa
kisheria maombi hayo yalipaswa yawasilishwe katika muda wa siku 60
tangu kutolewa kwa hukumu, lakini badala yake Tanesco iliwasilisha
maombi hayo baada ya siku 351.
Akizungumzia uamuzi huo, wakili Fungamtama alisema kuwa sasa Mahakama ya Rufani imefungua milango kwa Dowans kukazia hukumu ya Mahakama Kuu ili iweze kulipwa fidia kama ilivyoamuriwa awali.
Akizungumzia uamuzi huo, wakili Fungamtama alisema kuwa sasa Mahakama ya Rufani imefungua milango kwa Dowans kukazia hukumu ya Mahakama Kuu ili iweze kulipwa fidia kama ilivyoamuriwa awali.
Hii ni mara ya pili kwa Tanesco kushindwa
kusimamisha utekelezaji wa hukumu hiyo ya Mahakama Kuu. Mara ya kwanza
ilikuwa ni Septemba 6, 2012, baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es
Salaam kutupilia mbali maombi hayo.
Septemba 28, 2011, Mahakama Kuu iliiamuru Tanesco
kuilipa Dowans fidia ya Sh94 bilioni na riba ya asilimia 7.5, hadi
malipo ya mwisho yatakapokamilika, kufuatia tuzo iliyotolewa kwa Dowans
na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC).
ICC, katika hukumu yake ya Novemba 15, 2010, iliamuru Tanesco kuilipa Dowans fidia ya Dola za Marekani 65,812,630.03, kutokana na kuvunja mkataba wa kibiashara baina yake kinyume cha sheria.
ICC, katika hukumu yake ya Novemba 15, 2010, iliamuru Tanesco kuilipa Dowans fidia ya Dola za Marekani 65,812,630.03, kutokana na kuvunja mkataba wa kibiashara baina yake kinyume cha sheria.
Kufuatia uamuzi huo wa ICC, Dowans kupitia kwa
wakili wake Fungamtama iliwasilisha maombi Mahakama Kuu ya kusajili tuzo
yake iliyotolewa na ICC, ili utekelezwaji wa malipo hayo uweze kuwa na
nguvu ya kisheria.
MWANANCHI
MWANANCHI
Post a Comment