Itikadi za dini, siasa zatawala uchaguzi wa mabaraza
Uchaguzi wa Mabaraza ya Katiba katika ngazi ya
serikali za mitaa umnekamilika, kinachosubiriwa ni mikutano ya kata
kuteaua wawakilishi wa wane watakaoingia kwenye mabaraza ya wilaya.
Kwa mujibu wa mwongozo wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, wenyeviti wote na maofisa watendaji wa vijiji na mitaa
walishiriki kusimamia chaguzi hiyo na kuwaelekeza wananchi.
Hata hivyo, uchaguzi huo katika maeneo mbalimbali
ulitawaliwa na mgawanyiko kwa itikadi za kisiasa na kidini, ambako
wananchi walichaguana kwa kuangalia dini na vyama vyao.
Udini katika uchaguzi
Diwani wa Kata ya Kamachumu, mkoani Kegera, Dunstan Mutagahywa (CCM) ni miongoni mwa viongozi walioelezea tatizo hili baada ya kutembelea wilaya za Biharamulo, Muleba, Misenyi, Karagwe na Bukoba Vijiji.
“Nimegundua kuwa kampeni ya udini ilitawala sana
na kimsingi maeneo niliyozungukia nilibaini jinsi makundi mbalimbali ya
kidini yalivyokuwa yamejipanga kuwapigia kura waumini wao,” anasema.
Anasema jambo hilo limemfanya awe na wasi wasi wa
hali itakavyokuwa mwaka kesho na katika uchaguzi ujao, iwapo hali hiyo
isiporekebishwa.
“Uchaguzi Mkuu ujao hautakuwa kati ya CCM na vyama
vya upinzani, bali utakuwa kati ya ushindani wa wagombea wa dini moja
dhidi ya wale wa dini nyingine! Najiuliza tunakwenda wapi?” anahoji
katika ujumbe alioutuma kwa gazeti hili.
Mwenendo wa uchaguzi
Kabla ya kuanza kwa chaguzi hizo katika maeneo
mbalimbali, viongozi hao waliweka taratibu za watu kujiandikisha, katika
karatasi za mahudhurio na baadaye kuhakiki majina ya waliohudhuria,
kisha wananchi hao waliwapigia kura ya siri wagombea hao.
Hata hivyo mahudhurio hayakuwa makubwa wala
uchaguzi wenyewe haukuwa na hamasa, mathalan, katika Kata ya Kipawa
yenye wakazi 60,000 waliojitokeza kupiga kura walikuwa 1,181 na jumla ya
wagombea walikuwa 148.
Maoni ya wananchi
Omari Aly Dodo mkazi wa Kipawa, Dar es Salaam anasema uchaguzi haukupangiliwa vizuri lakini wapiga kura walikuwa waelewa na kwa jitihada za oaofisa watendaji walifanikisha uchaguzi huo.
‘’Uchaguzi sio kitu cha kubahatisha, na hili Tume
imeonyesha kufanya mambo kwa kubahatisha na bila kujipanga maana
hawakutoa karatasi za kupiga kura wala maelekezo ya kina juu ya uchaguzi
huu. Ndani ya kata mmoja uendesha wa uchaguzi umetofautiana, hali hiyo
sio picha nzuri,” anasema Dodo.
Mkazi mwingine wa kata hiyo, Rutashobya Rutasobya anasema ingawa
uchaguzi umekuwa huru na haki lakini hakukuwa na utaratibu mzuri wa
kufanisha uchaguzi huo.
Naye Fredrick Kabati kutoka mtaa wa Karakata
anasema kumwanchia ofisa mtendaji wa mtaa na mwenyekiti pekee kusimamia
wananchi karibia 386 haikuwa sawa.
Katika suala la utaratibu, Kabati anasema pia siku yenyewe ya uchaguzi haikuwa sahihi maana ilikuwa ni siku ya kazi, ambayo imesababisha watu wengi kutohudhuria.
Katika suala la utaratibu, Kabati anasema pia siku yenyewe ya uchaguzi haikuwa sahihi maana ilikuwa ni siku ya kazi, ambayo imesababisha watu wengi kutohudhuria.
Mkazi mwingine wa kata hiyo, Simoni Makabwa,
anasema uchaguzi umefanyika huru na haki ukiachilia changamoto kadhaa
zilizojitokeza, lakini anawapongeza wenyeviti wa mitaa na maofisa
watendaji wa mitaa kwa kutumia jitihada zao kufanikisha uchaguzi.
Makabwa anatoa angalizo wakati kuchuja majina hayo
nakubakiza majina manane ya mtaa, basi kuwepo na maslahi ya Taifa
kwanza ili wapatikane watu sahihi.
’Maana hatuja ambiwa watu hao nane wa kata
watapatikana kwa sifa zipi basi tunaomba hao wajumbe waongozwe na
uzalendo kwa ajili ya nchi yetu,” anasema Makwaba.
Rukia Chacha, Mwenyekiti wa Mtaa wa Mogo anawashukuru wananchi wa Mtaa wa huo kwa “kujitokeza kwa wingi na kufanikisha tukio hilo” lakini akasema wamekumbana na changamoto nyingi.
Rukia Chacha, Mwenyekiti wa Mtaa wa Mogo anawashukuru wananchi wa Mtaa wa huo kwa “kujitokeza kwa wingi na kufanikisha tukio hilo” lakini akasema wamekumbana na changamoto nyingi.
“Hakukuwa na maandalizi, pili vifaa vya uchaguzi
kwa maana ya makaratasi na hata masanduku na sehemu ya kupigia kura
ilikuwa changamoto,” anasema Chacha.
Mtendaji wa Mtaa wa Karakata Cecilia Chausi
anasema uchaguzi umeenda salama, ingawa kulikuwa na mabishano ya hapa na
pale, changamoto kubwa imekuwa katika vifaa vya uchaguzi, ambapo
walilazimika kutumia fedha zao kufanukisha jukumu hilo.
Kwa upande wake Latifa Mlawa, ofisa mtendaji wa
mtaa wa Kipunguni anasema ingawa uchaguzi ulifanyika salama katika mtaa
wake lakini changamoto kubwa ilikuwa maandalizi yake duni.
“Tume ya Mabadiliko ya Katiba haikuwashirikisha
wadau wa uchaguzi huo, hasa maofisa watendaji wa mtaa na wenyeviti wa
mitaa ndio maana changamoto zilikuwa nyingi na tumeendesha chaguzi hizi
kwa busara yetu,” anasema Mlawa.
Wananchi mbalimbali waliohojiwa wanansema ili
uchaguzi uonekane ni mzuri Tume ilikuwa na wajibu wa kuweka utaratibu
mmoja wa jinsi ya kuwachagua wajumbe hao.
Wanasema pia Tume ilitakiwa kuweka muda mmoja na
siku moja kwenye kata nzima ilikuwadhibiti wapiga kura kushiriki zaidi
ya sehemu moja.
Kuhusu mahudhurio hafifu, wananchi hao wanasema uhamasishaji ulikuwa mdogo na siku ya kazi.
Nachingwea na itikadi za vyama
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nachingwea Mkoani Lindi, Rajabu Macholilo anasema uchaguzi umefanyika salama ingawa kulikuwa na changamoto kadhaa ikiwamo wananchi kuchaguana kwa kuangalia vyama badala ya maslahi ya Taifa kwanza.
Nachingwea na itikadi za vyama
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nachingwea Mkoani Lindi, Rajabu Macholilo anasema uchaguzi umefanyika salama ingawa kulikuwa na changamoto kadhaa ikiwamo wananchi kuchaguana kwa kuangalia vyama badala ya maslahi ya Taifa kwanza.
Kata yake inajumuisha vijiji vitatu vya Kilimahewa, Nachingwea na Dodoma.
Akifafanua anasema kulikuwa na changamoto ya
mahudhurio na cha ajabu katika Kijiji cha Kilimahewa hakuna mwanamke
hata mmoja aliyejitokeza kugombea.
Anasema katika Kijiji cha Nachingwe wanawake walijitokeza lakini hawakupata kura hata moja.
MWANANCHI
Anasema katika Kijiji cha Nachingwe wanawake walijitokeza lakini hawakupata kura hata moja.
MWANANCHI
Post a Comment