KAMANDA WA POLISI DODOMA AKUTANA NA KUONGEA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA TARAFA YA DODOMA MJINI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma DAVID MISIME - SACP akiongea na Viongozi mbalimbali wa Tarafa ya Dodoma Mjini na kutoa maelekezo ya ulinzi na usalama.
Afisa tarafa Dodoma Mjini HEMEDI HUSSEIN na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma DAVID MISIME - SACP wakisoma baadhi ya maelekezo kwa viongozi wa Kata na Vitongoji vya Dodoma mjini alipokutana na viongozo hao.
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Mch. JOSHUA MTAKYAMA wa KKKT Nkuhungu Dodoma akichangia jambo katika kikao hicho.
Viongozi mbalimbali wakimsikiliza kwa makini Kamanda wa Polisi Moa wa Dodoma David Misime - SACP.
Na: Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi DAVID
MISIME – SACP amesema jukumu la kwanza la serikali za mitaa ni
kuwahakikishia wananchi wake usalama, amani, utulivu na utengamano hivyo
ni jukumu la watendaji wa kata, mwenyekiti wa Mitaa na vitongoji
kusaidia kuimarisha ulinzi katika maeneo yetu.
Amesema
hayo alipokutana na Viongozi wa mbalimbali wa Tarafa ya Dodoma mjini
katika Ukumbi wa Polisi Dodoma wakiwemo Madiwani, Afisa tarafa,
Watendaji wa Kata, Wenyekiti wa Serikali za mitaa, Vitongoji na Viongozi
wa Dini na kusisitiza masuala ya ulinzi na usalama katika kipindi hiki
cha tukio la kihistoria la kupata Katiba mpya.
Kamanda
MISIME ameongeza kuwa kuwaambia wenyekiti wa serikali za mitaa
kuvifufua vikundi vya ulinzi shirikishi hasa katika kipindi hiki cha
mchakato wa kupata katiba mpya ili kuweza kuzuia uhalifu hasa wa
uvunjaji.
Aidha
Kamanda MISIME amewaomba viogozi hao kushirikiana katika kupunguza
ajali za usalama barabarani pamoja na kujenga utamaduni wa kusema
familia yangu haina uhalifu.
Pia
Kamanda MISIME amewataka wamiliki wote wenye baa na Kumbi za starehe
kuzingatia sheria za kufungua na kufunga baa na kumbi hizo kwani
zimekuwa ni sehemu ya maficho ya wahalifu.
Post a Comment