MUGABE ATIMIZA MIAKA 90, SHEREHE YAKE KUFANYIKA UWANJANI JUMAPILI, ITATUMIA DOLA MIL 1, AFYA YAKE YADODA


Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe leo anasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza umri wa miaka 90. Hata hivyo sherehe yake imegubikwa na wasiwasi juu ya afya yake.
Wakati ambapo wasaidizi wake wanasema afya yake iko vizuri, wiki hii alienda tena nchini Singapore kwaajili ya upasuaji wa macho na hivyo kuamsha tena wasiwasi. Bado yupo nchini humo na sherehe yake ya kuzaliwa itafanyika uwanjani siku ya Jumapili na inadaiwa kugharimu dola milioni 1.
Kiongozi huyo wa Zimbabwe tangu mwaka 1980, amekuwa akienda Singapore kutibiwa mara kadhaa.
Mugabe alizaliwa tarehe 21 February 1924. Sherehe yake itahudhuriwa na maelfu ya wananchi kwenye uwanja wa Marondera, mji uliopo kilomita 75 mashariki mwa mjini mkuu, Harare.
Kutakuwepo na muziki, michezo na chakula.

No comments

Powered by Blogger.